google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 28, 2016

Hawa Ndio Watu Ambao Hawadumu Sana Katika Ndoa Zao.

No comments :
Baada ya kusemwa kama hadithi, hivi sasa imethibitika kwamba, watu wanaooana kwa sababu ya kuvutana kimwili, kimtazamo, imani za dini zao na nasaba wanazotoka, hawawezi kudumu kwenye ndoa kama tabia zinatofautiana.
Kuna watu ambao huoana kwa sababu tu ni waumi wa dhehebu moja. Wengine huoana kwa sababu wazazi wao wanatoka kwenye familia za kiwango cha juu kimapato au kisomi, ama kiwango cha chini. Wengine huona kwa sababu wana mitazamo ya aina moja kwenye jambo fulani. Huku wengine wakiona kwa sababu ni kabila moja.
Imethibitika sasa kwamba, nusu ya ndoa zinazofungwa kwa sababu hizo, huwa hazidumu. Tafiti kadhaa zinaonesha kwamba, ndoa zinazodumu ni za wale watu ambao wameoana kwa sababu kila mmoja amezijua tabia za mwingine na kukubaliana nazo.
Lakini kikubwa kilichobainika ni kwamba, wanaooana  na kudumu kwenye ndoa, ni wale ambao wanalingana tabia kwa sehemu kubwa. Bila kujali kila mmoja anatoka na familia ya namna gani, dini au mitazamo, tabia zikikaribiana kulingana, uwezekano wa kuishi katika ndoa ya amani ni mkubwa sana.

TABIA NJEMA KWENYE NDOA NI MUHIMU SANA.
Kwa kuwa ni vigumu sana kwa watu kujua tabia zao, kuoana kwingi kumefungwa kwenye vigezo nilivyovitaja ambavyo ni muda. Baada ya muda fulani kwenye ndoa, wanandoa hugundua kwamba, vigezo vilivyotumika kuwaunganisha, havina uwezo wa kuwafanya wadumu tena kwenye ndoa hiyo.
Hii ina maana kwamba, wapenzi wanapokuwa na tabia zinazokaribiana, ndoa yao pia inaweza kuwa imara zaidi. Lakini wapenzi kuunganishwa na dini zao, hadhi yao katika jamii na mitazamo fulani, haiwezi kuwahakikishia wanandoa kuwa na ndoa imara.
Mitazamo fulani ya aina moja, imani ya dini au kiwango sawa cha kipato kifamilia, huwavuta watu awali wanapokutana na kuoana. Hii inatokana na ukweli kwamba, sifa hizi huonekana haraka na ni sifa muhimu kwa watu wengi katika kuendesha maisha yao, wakati tabia zimejificha.
Huchukua muda kwa mtu kugundua tabia halisi za mwingine. Bahati mbaya sana mtu anapohisi kwamba fulani amempenda, huweza kuficha udhaifu wake kitabia na hivyo kuwa ngumu zaidi tabia kuchukuliwa kama kigezo, wakati ndicho kigezo halisi kinachotakiwa kutazamwa kabla watu hawajaamua kuoana.
Lakini bahati mbaya ni kwamba, kwa kadri watu wanavyozidi kuishi kwenye ndoa, ndivyo tabia zinavyojitokeza na kuwa muhimu sana katika kuimarisha ndoa hiyo. Kwa hiyo, kama tabia hazifanani, ina maana kwamba, kadri siku zinavyoenda, ndivyo wanandoa wanavyozidi kushindana.
Uhusiano imara na wenye faraja unahitaji mawasiliano ya mara kwa mara kuhusiana na shughuli za wanandoa, masuala mbalimbali, matatizo na suluhu za mambo mengi ya kimaisha. Kama tabia za watu wawili haziwiani katika mambo, ni wazizi kutakuwa na tatizo.
Baadhi ya watafiti wanasisitiza kwamba watu wote ambao wanaingia kwenye ndoa huku wakijua kwamba kitabia hawakaribiani, ni sawa na kupiga mbizi baharini wakati mtu hajui kuogelea.
Pale ambapo watu wanataka kufunga ndoa, wanaona wazi wazi kuwa kitabia ni watu wawili tofauti sana, hawashauriwi kuendelea na zoezi hilo kwani litawaumiza vibaya sana hapo baadae.
Kama tabia zinalandana sana, bila kujali kama ni watu wadini moja, uwezo sawa wa kifamilia, kabila moja na mitazamo fulani ya aina moja, watu hao hao wanaweza kutabiriwa bila wasiwasi kwamba, ndoa yao itadumu.
Nikutakie siku njema na mafanikio bora katika ndoa yako. Endelea kujifunza kupitia DIRAYA MAFANIKIO kila wakati.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani ngwangwalu,
Kama una maswali, changamoto au unahitaji ushauri uwe wa kibiashara/maisha, usisite kuwasiliana nasi kwa:-
Simu0713 048 035,
E-mail; dirayamafanikio@gmail.com



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.