google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 22, 2017

Haya Ndiyo Mahusiano Yaliyopo Kati Ya Mafanikio Na Afya Yako.

No comments :
Je kuna mtu ambaye hapendi mafanikio katika maisha yake? Kila mtu ukimuuliza atakwambia ana taka mafanikio, maendeleo na maisha bora.
Lakini ulisha wahi kujiuliza afya yako ina husiana vipi na mafanikio unayoyahitaji? Je una weza kufanikiwa bila kuwa na afya bora na imara? Haya ni baadhi ya maswali ya msingi unayopaswa kuji uliza kabla huja endelea kusoma makala hii.
Tabia zetu zimekua zikiathiri moja kwa moja afya yetu hivyo kupelekea kushindwa kutimiza malengo tunayo jiwekea katika maisha yetu. Tabia hizo ni vitu ambavyo tunaviendekeza na kuvichukulia kama sehemu ya maisha yetu bila kujua madhara yake baadae.
Tofauti kati ya bustani na msitu ni matunzo, bustani hutunzwa hivyo hustawi na kupendeza na kuifanya izae matunda mazuri yapendezayo. Hivyo mwili nao unahitaji matunzo ili uweze kukupa matunda unayo tamani.
TABIA ZINAZO ATHIRI AFYA ZETU
1. Ulaji Mbaya Wa Chakula.
Hapa ndipo watu wengi wana angukia, kuna makundi mawili ya ulaji mbaya
Ratiba mbaya ya kula
Watu wengi hawana ratiba nzuri ya kula na wengi huchelewa kula kwa madai kazi zina watinga. Lakini ukweli ni kuwa ukichelewa kula una ua mwili wako taratibu, magonjwa kama vidonda vya tumbo yamekua yaki wasumbua watu wengi kutokana na kushindwa kula kwa wakati.
Kula usiku sana hupelekea mwili kutunza mafuta na kuongezeka uzito. Kupoteza uwezo wa kufikiri,na kusinyaa kwa ubongo kutokana na kukosa cha nguvu kwa muda mrefu.
Kula vyakula hatarishi
Ulaji wa vyakula vya sukari kwa wingi,chumvi na kahawa hupelekea magonjwa kama shinikizo la damu na kusukari pia kuongezeka uzito kupunguza uwezo wa moyo kufanya kazi na kuathiri uwezo wa kufikiri.
CHAKULA BORA NI MAFUTA YA UBONGO.
Kula chakula bora kwa afya yako.
2. Msongo wa mawazo.
Ndio msongo wa mawazo, kuwaza ni kitu cha kawaida kwa mwanadamu. Lakini kuwaza kupitiliza husababisha matatizo makubwa bila kujijua.
Vitu kama kufanya kazi kupitiliza, majibizano,kukosa muda wa kutosha kupumzika, kukataliwa huweza kusabisha msongo wa mawazo.nakuleta madhara kama kupoteza mwelekeo, kushindwa kufanya maamuzi,kupoteza umakini,kushindwa kuhusiana na watu vizuri.
3. Kukosa Muda mzuri wa Kulala.
Uta shangaa kulala? lakini ukweli unabaki pale pale, kulala kwa wakati. Una lala saa kumi na kuamka saa kumi na moja hii ni moja kati ya tabia hatarishi sana kwa afya zetu. Wanasayansi wana shauri kulala kwa afya ni masaa 6-7.
Magonjwa ya figo,moyo,uzito ulio pitiliza,kisukari na shinikizo la damu yana weza kusababishwa na kukosa muda wa kutosha kulala.
4. Tabia binafsi.
Hizi ni zile tabia ambazo mtu huzi anzisha na baadae kushidwa kuzi himili na huanza kumuendesha, tabia kama ulevi,kuvuta sigara,madawa ya kulevya,ngono zembe,huanza taratibu na baadae hugharimu afya yako.
Watu wotewalio fanikiwa hujali afya zao kuliko mali walizo nazo, lakini maskini hutumia kidogo alicho nacho kuharibu afya yake bila kujua, na huku aki hitaji kufanikiwa.
HUWEZI KUPATA MAENDELEO KAMA HUTA ITUNZA AFYA YAKO.
ITUNZE AFYA YAKO KWA MAENDELEO YAKO.
Makala imeandikwa na Dr.Julius Kimaro, 0745524031.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.