google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 31, 2017

Toka Kwenye Vifungo Hivi,..Utengeneze Zaidi Mafanikio.

No comments :
Vipo vifungo vingi ambavyo vinaweza kukufunga na kukupotezea mafanikio yako. Vifungo vingine unavijua na vingine unaweza ukawa huvijui. Kwa mfano;-
Acha kujiweka kwenye vifungo vya kidini na kuamini utajiri mkubwa ni dhambi. Kumbuka, mafanikio hayana uhusiano moja kwa moja na kutenda mabaya.
Acha kuamini umaskini ndio ni kitu kizuri kwako. Hivyo ukashindwa kuweka juhudi zako zote kwa kisingizio cha kwamba ukiwa maskini ni sawa kwako.
Acha kuamini ukiwa na pesa nyingi ndio ushetani. Utajikwamisha sana wewe mwenyewe kufikia mafanikio yako bila kujijua ukiwa upo kwenye kifungo cha dini.

Acha kuamini kwamba Mungu atakusaidia kila kitu, hata kama umebweteka na wala hujitumi sana yaani huweki juhudi sana, ndio maana amekupa akili ufikirie na vingine.
Acha kutumia uvivu wako kutumia kama kisingizo ukiamini hio ndiyo imani sahihi.. Kama kuna kazi unayotakiwa kufanya, fanya kweli. acha kuendekeza uvivu unaomba kazi kwenye kampuni moja halafu unamlaumu Mungu. Ukiona uko hivyo ujue kabisa upo kwenye kifungo..
Toka kwenye kila aina ya vifungo ambavyo unaona vinakukwamisha kufanikiwa sana kwenye maisha yako, kuwa huru ili utengeneze mafanikio yako.
Kila la kheri katika kufikia mafanikio  makubwa.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 628 929 816, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.