google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 14, 2015

Mambo 4 Unayotakiwa Kuyajua Kuhusu Pesa, Ili Uwe TAJIRI.

1 comment :
Ikiwa wewe ni mmoja wa watu wanaotaka kufikia mafanikio makubwa na hatimaye kuufikia utajiri ni muhimu kujua sifa, tabia, kanuni za pesa na hata mambo mengi yanayohusu pesa. Hilo litakusaidia sana kuweza kuitawala na kutobabaika nayo pale inapokuwa mfukoni mwako na isitoshe kwa kujua sifa, tabia, kanuni au mambo hayo itakusaidia wewe hata kuzilinda na kuwa nyingi zaidi.
Bila shaka umewahi kusikia watu ambao wanapesa nyingi sana leo, lakini baada ya muda fulani unakuja kusikia tena watu wale hawana hizo pesa katika maisha yao. Kitu kinachotokea hapo kikubwa ni kutokana na ukosefu wa kutokujua mambo muhimu yanayoihusu hiyo pesa na siyo kingine. Matokeo yake inakuwa ni upotevu wa pesa nyingi.
Ili uwe tajiri, mbali na kujua mbinu za kutafuta pesa ambazo tumekuwa tukiziongelea sana humu ndani, lakini ni lazima kwako pia kujua misingi au mambo muhimu yaliyo katika pesa hiyo unayoitafuta katika maisha yako. Haya ni mambo ambayo yatakusaidia kukuza uelewa wako juu ya pesa lakini si hivyo tu yatakusaidia pia kukupa nguvu ya kuzisaka, kuzitafuta na hata kufikia mafanikio makubwa.
Yafuatayo Ni Mambo 4 Unayotakiwa Kuyajua Kuhusu Pesa, Ili Uwe TAJIRI.
1. Pesa ni uhuru.
Hakuna uhuru wa kweli utakoupata kwenye maisha yako kama utakuwa huna pesa. Unapokuwa na pesa inakufanya uwe huru sana katika maisha yako. Hiyo ni kwa sababu unapokuwa na pesa itakufanyia mambo mengi ikiwa pamoja na kupata chakula kizuri unachotaka, utasafiri na hata kupata matibabu vizuri. Kukosa pesa ni utumwa tena mkubwa ambao unaambatana na manyanyaso. Ni muhimu kulijua hili ili kuongeza kasi ya kutafuta pesa zaidi na kondokana na utumwa huo.

2. Tumia pesa yako kulingana na kipato chako.
Haina maana katika maisha yako kama utakuwa unatumia kiwango kikubwa cha pesa kuliko kile unachokipata. Kitu ambacho unatakiwa kuhakikisha ni kutumia pesa sawasawa na kipato chako. Kama yapo matumizi yasiyo ya lazima yaondoe. Kwa kulijua hili itakupelekea kutunza pesa nyingi ambazo zitakusaidia kuwekeza katika maeneo mengine.
3. Itumie pesa yako katika uwekezaji.
Kila pesa unayoipata, fanya kila uwezalo nyingine iweke pembeni kwa ajili ya suala zima la uwekezaji. Acha kutumia pesa yako yote katika kula tu peke yake. Ikiwa utatumia pesa yote katika kula na kusahau kuwekuza tambua kabisa unajitengenezea njia mwenyewe ya kuelekea kwenye umaskini. Hili ni jambo muhimu pia kulijua kuhusu pesa litakusaidia kuwa makini sana katika matumizi kwa ujumla.
4. Wekeza pesa yako katika maeneo tofauti.
Katika uwekezaji ambao tumetoka kuongelea hapo juu, usiwekeze pesa zako katika eneo moja tu. Kwa jinsi utakavyozidi kuendelea kukua kifedha wekeza katika maeneo taofauti tofauti ili kuwa na vitega uchumi vingi vitakavyokuingizia pesa. Ikiwa utawekeza katika eneo moja ikitokea umekwama basi mambo yote yanakuwa yameishia hapo.
Kwa vyovyote vile unahitaji kujifunza mambo mengi yanayohusiana na fedha ili kuweza kufanikiwa zaidi. Kwa kuanzia nimekupa mambo hayo machache ili kukujengea misuli ya kusonga mbele.
Nakutakia ushindi katika safari ya mafanikio yako na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nami kwa email dirayamafanikio@gmail.com au simu 0713 048035 kwa ushauri na msaada wa haraka.  








1 comment :

Note: Only a member of this blog may post a comment.