google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 9, 2015

Hivi Ndivyo Vizuizi Vikubwa Vinavyokufanya Ushindwe Kufanikiwa.

No comments :
Wengi wetu siku zote huwa ni watu wa kutafuta mafanikio. Jambo hili tunakuwa tunaliona hasa  kutokana na shughuli zetu tunazozifanya kila siku ambazo zinakuwa zinalenga mafanikio hayo tunayoyataka. Hakuna mtu ambaye anakuwa hatamani mafanikio, kila mtu anakuwa ana hamasa ya kutaka mafanikio katika maisha yake tena kwa nguvu zote bila kuchoka.
Lakini pamoja na wengi wetu kuwa na nia hii ya kutaka mafanikio hayo, huwa siyo rahisi kuyafikia. Hili mara nyingi linakuwa linatokea hivyo kutokana na safari ya mafanikio kuwa na changamoto zake ama vizuizi ambavyo ni lazima uvivuke ili kufanikiwa. Wengi wanapokutana na vizuizi hivi hujikuta wamekwama na unakuwa ndiyo mwisho wao hapo.
Inapotokea umekutana na vizuizi hivi visije vikakufanya ukabaki na huzuni na kujiona hufai tena ama una mkosi. Kitu kikubwa cha kufanya jifunze, kisha chukua jukumu la kusonga mbele. Tambua, ni lazima kuvielewa vizuizi hivi ili kujua namna ya kukabiliana navyo na kwenda upande wa pili wa mafanikio, la sivyo utakwama kila siku.
Je, ni vizuizi vipi hivi?
1. Kukosa mipango na malengo.
Watu wengi wamekuwa wakishindwa kufikia malengo yao makubwa kutokana na kukosa mipango na malengo iliyothabiti. Hiki ni kitu ambacho kimekuwa kikiwakwamisha watu wengi sana katika safari yao ya mafanikio. Ili kuweza kufanikiwa ni lazima kuwa na mipango na malengo imara. Kuwa na mipango na malengo ndiyo dira yako kubwa ya kukufanikisha.
Huwezi kufanikiwa kwa lolote kama utakuwa huna vipaumbele unavyotakiwa kuvitekeleza. Siri kubwa ya mafanikio ipo kwenye vipaumbele unavyojiwekea katika maisha yako kila siku. Kizuizi kimojawapo kinachopolekea ndoto za wengi kutokutimia ni kushindwa kujiwekea vipaumbele hivi, ambavyo ni muhimu kwa mafanikio yao.
3. Kuahirisha mipango.
Hili ni tatizo kubwa sana linalowakabili wengi wetu bila kujijua. Wapo watu ambao mara nyingi wanatabia ya kusema nitafanya hiki kesho, na inapofika kesho hiyo hawafanyi tena. Watu hawa hujikuta ni watu wenye kuahirisha  mambo mengi sana karibu kwenye kila jambo kwenye maisha yao. Kwa tabia hii ya kuahirisha mipango yao wamekuwa wakijiwekea kizuizi kikubwa kwenye mafanikio yao bila kujua na malengo yao kutotimia kabisa. Ili kufanikiwa ni muhimu kuachana na tabia ya kuahirisha mipango.
4. Kukosa nguvu ya uzingativu.
Pia hiki ni chanzo kikubwa cha malengo mengi ya watu kutokuweza kutimia katika maisha yako. Kwa kawaida ili uweze kufanikiwa unahitajika kuweka nguvu zako nyingi za uzingativu katika eneo moja mpaka upate kile unachokihitaji au matokeo unayoyataka. Sasa tatizo la wengi hawafanyi hivi na matokeo yake kusababisha malengo yao kutotimia siku zote.
5. Kuacha kushikiria malengo mpaka mwisho.
Wengi linapotokea tatizo huwa ni rahisi sana kwao kushindwa kung’ang’ania malengo yao mpaka kupata kile wanachokihitaji. Wengi hujikuta ni watu wa kuishia kati na kukata tamaa. Kwa mtindo huu wa maisha suala la kufanikiwa linakuwa gumu sana kuwezekana. Hii ni kwa sababu mafanikio yanataka kwa kiasi kikubwa uwe na uwezo wa kung’ang’ania mpaka ufanikiwe. Kinyume cha hapo sahau mafanikio hayo.
6. Kutokujitoa.
Kujitoa ni moja kati nguzo kubwa sana ya mafanikio katika maisha ya mwanadamu. Wengi wetu huwa ni watu wa kutaka mafanikio bila kujitoa kikamilifu ili kufikia mafanikio hayo. Kama unaishi maisha haya ya kutokujitoa suala la kuwa na mafanikio makubwa katika maisha yako litakuwa kigumu kidogo kutokea.
7. Kukosa mafunzo.
Kutokana na wengi kukosa mafunzo muhimu ya kuwasaidia kufanikiwa hujikuta ni watu wa kukwama kila siku katika maisha yao. Ili uweze kufanikiwa unahitajika kujifunza kila siku. Kujifunza huko unatakiwa kujifunza kupitia vitabu, semina na warsha mbalimbali ambazo zinaweza zikawa ni muhimu kwako ili kuleta mabadiliko ya kweli kwenye maisha yako.
8. Kukataa mabadiliko.
Haiwezekani hata kidogo ukaweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa ikiwa wewe mwenyewe hutaki kutambua mabadiliko muhimu yanayoendelea katika maisha ya kila siku. Maisha yanabadilika na yataendelea kubadilika siku zote. Hivyo ni lazima kwako kuweza kubadilika ili kuendana na kasi ya maisha, vinginevyo utaachwa nyuma sana kiasi kwamba utabaki unashangaa.
9. Kukata tamaa.
Hiki pia ni kizuizi kikubwa sana ambacho wengi kinawakwamisha katika harakati zao za kuelekea kwenye mafanikio. Wengi wetu huwa ni watu wa kukata tamaa tunapokutana na magumu. Hali hiyo inapojitokeza suala la kusonga mbele na kufanikiwa linakuwa siyo rahisi hata kidogo kuweza kutokea katika maisha yako.
10. Hofu ya kushindwa.
Wapo watu ambao mara nyingi huwa na nia ya kufanikiwa, lakini kinachowazuia kufanya hivyo ni kutokana na ile hofu yao kubwa waliyonayo ndani mwao ya kuogopa kushindwa. Hofu hii mara nyingi inakuwa inajitokeza pale unapotaka kufanya jambo jipya. Kwa kuwa na hofu hii tu, wengi hujikuta wamekwama kufikia malengo yao makubwa.
Kushindwa kwa mtu katika maisha yake mara nyingi kunasababishwa na vizuizi vingi sana ikiwemo hivyo ambavyo tumejifunza. Bila kuwa makini na kuchukua hatua imara za kukabiliana na vizuizi hivyo, itakuwa ni kitu kisichowezekana kuyafikia mafanikio unayoyahitaji siku zote. Chukua hatua na tafakari.
Nakutakia ushindi katika mabadiliko juu ya maisha yako na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 04 80 35,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.