google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 8, 2015

Jinsi Ya kuweka Vipaumbele Katika Malengo Hadi Kuyafikia.

1 comment :
Kila mtu ili kuweza kufikia mafanikio ni muhimu kwake kujiwekea malengo. Malengo haya anayojiwekea huwa ni lazima kuyatimiza. Inapofika mahali ukawa ni mtu wa kushindwa kutimiza malengo yako mara kwa mara, hiyo inakuwa ni hatari na shida kwako kuelekea kwenye safari ya mafanikio. Jaribu kujiuliza pale unapokuwa hutimizi malengo yako huwa unajisikiaje? Bila shaka ni vibaya.
Lakini hata hivyo pamoja na kujiwekea malengo hayo kuna wakati huwa tunajikuta tunakuwa tunamalengo mengi ambayo huanza kutuchanganya na kushindwa kujua tufanye lipi kwanza na tuache lipi. Kwa mfano, katika hali ya kawaida unaweza ukajikuta una malengo mengi zaidi ambayo umepanga na unatakiwa kuyatekeleza, hapo unafanyaje?
Kwa kawaida malengo yanapokuwa mengi unakuwa huna uwezo wa kuyatekeleza yote kwa pamoja hata ungefanyaje? Hii yote huwa inatokea hivyo kwa sababu, kila lengo linakuwa linachukua muda na nguvu kulitekeleza hadi kufanikiwa. Hivyo malengo yanapokuwa mengi inakuwa siyo rahisi kufanikiwa kutokana na sababu hiyo.
Na hata kama ikatokea umejaribu kufanya malengo mengi kwa wakati mmoja basi utafanya kwa uhafifu badala ungefanya malengo machache na kwa ubora wa hali juu kabisa. Utafanya vizuri kwenye malengo ikiwa utajitoa kwenye malengo machache( Pengine moja) yaliyofafanuliwa na kupangwa vyema kabisa.

Sasa, una malengo mengi na unataka kweli kuyatimiza yote hapa unafanyaje? Unachotakiwa kufanya ni kuweka vipaumbele. Hakuna njia nyingine ya mkato unayoweza kuitumia vinginevyo utashindwa kufikia malengo yako.
Kwa mfano, unaweza ukajikuta una malengo ya kutimiza kumi katika kipindi cha muda fulani. Hapo kwanza, katika hali ya kawaida huwezi kutimiza malengo yote kumi kwa wakati mmoja, ila unachotakiwa kufanya ili malengo yako hayo yatimie ni kuweka kipaumbele tena kwa haraka sana.
Pengine unajiuliza, nitawekaje kipaumbele? Nitakueleza unachotakiwa kufanya.  Unachotakiwa kufanya ni kujiuliza swali hili ‘ Kama nitaacha kila kitu isipokuwa kimoja katika malengo yangu niliyonayo, ni kitu gani kimoja ambacho ningeanza kukitekeleza?’ Utakapojibu swali hilo hicho ndicho kipaumbele mbele chako cha kwanza unachotakiwa kukitekeleza bila kuacha.
Kwa lugha nyingine hapo katika uwekaji wa vipaumbele chagua kile kilicho cha muhimu kuliko vingine vyote anza kukitekeleza. Kitu hicho kikishakamilika nenda kingine tena. Kwa kufanya hivyo utajikuta malengo yako yanatimia moja baada ya jingine na mwisho wa siku utajikuta malengo yote yametimia. Acha kubabaika na uzuri wa malengo mengine, ukishaweka kipaumbele, fata lengo moja tu, mpaka litimie.
Acha kujifanya kutekeleza malengo yote kwa wakati mmoja hutaweza na itafika mahali lazima utakwama tu. Nguvu yako kubwa ya kukufanikisha hasa pale unapokuwa na malengo mengi ni kufanya lengo moja moja kwanza. Hiyo ndiyo siri ya ushindi ilioyopo katika uwekaji wa vipaumbele.
Hivyo, watu ambao wataweza kuyapa vipaumbele malengo yao. Katika maana halisi na mtiririko mzuri ni wazi kuwa lazima watafanikiwa. Chukua hatua hii ya kuweka vipaumbele katika malengo yako ili ufanikishe, kufaulu na kusonga mbele kwa ujasiri. Tegemea mafanikio makubwa kama utatekeleza hili.
Tunakutakia kila la kheri katika safari ya mafanikio, endelea kuwashirikisha wengine kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kila siku kwa kujifunza na kuhamasika zaidi.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 04 80 35,





1 comment :

  1. Mawazo mazuri sana tukizingatia tufafikia ndoto au shabaha zetu. ipo poa sana

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.