google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 19, 2015

Haya Ndiyo Mabadiliko Ya Lazima Unayotakiwa Kuyafanya Sasa Ili Kufanikiwa.

No comments :
Hakuna mtu ambaye anapenda kuona maisha yake yakienda hovyo ama akiwa hana kipato cha kutosha. Kila mtu mpenda mafanikio huwa ana nia ya kutaka kufanikiwa na kuona mambo yake yakienda sawa kama anavyotaka iwe kwake. Lakini maisha hayo ya mafanikio huwa hayawezi kuja hivihivi tu, ni lazima kuwe na mabadiliko ambayo yanatakiwa kufanyika.

Kwa kufanya madiliko hayo muhimu ni lazima kwa vyovyote vile maisha yako yatabalika. Acha ile tabia ya kukaa na kuanza kulalamika, unachotakiwa kufanya wewe ni kuleta mabadiliko yatakayokutoa sehemu moja na kukupeleka nyingine na siyo kulalamika. Haya ndiyo mabadiliko unayotakiwa kuyafanya katika maisha yako. Je, ni mabadiliko gani kwako ya lazima ambayo unatakiwa kuyafanya ili kufanikiwa zaidi?

1. Kuwa mtu wa vitendo.
Kitu kitakachoweza kukufanikisha na kukutoa hapo ulipo ni kwa wewe kuwa mtu wa vitendo. Watu wengi ambao hawana mafanikio huwa ni watu ambao ni waongeaji sana juu ya ndoto zao lakini si watendaji. Mabadiliko unayotakiwa kuyafanya wewe ni kuwa mtendaji, hata kama ni kwa kidogo wewe tenda na acha kuahirisha mipango yako mara  kwa mara. Kwa kuwa mtu wa vitendo ni lazima uone mabadiliko.



2. Kuwa king’ang’anizi.
Katika safari ya kutafuta mafanikio mara nyingi huwa tunakutana na vikwazo vingi ambavyo vingine hutukatisha tamaa sana. Lakini lilokubwa kwako ni kuwa king’ang’azi kwa kushikilia ndoto zako mpaka kuona zinaleta majibu. Kama umefika mahali umekwama acha kukataa tamaa mapema jipe moyo kisha zidi kusonga mbele, safari bado inaendelea na fanya mabadiliko haya ya kuwa king’ang’azi utaona mabadiliko.

3. Kuwa na mipango inayoeleweka.
Katika hili ili uweze kufanikiwa hakikisha uwe unajua unatoka wapi na unakwenda wapi na kwa muda gani. Hakikisha uwe unajua ni nini unachotakiwa ufanye kwa siku, wiki, mwezi na hata mwaka ili kutimiza malengo uliyojiwekea. Haya yote yatawezekana kwa kupangilia vizuri. Haya ni mabadiliko ya lazima unayoyahitaji kwani bila utaratibu huu utakuwa unaishi hovyo na itakuwa ngumu sana kwako kufikia malengo yako.


4. Kuwa makini na afya yako.
Wengi huwa ni watu ambao hawaelewi sana juu ya hili. Kitu cha pekee ambacho kinaweza kukusaidia kufikia ndoto zako ni afya yako. Kama utakuwa na afya mbovu, hata uwe na ndoto nzuri vipi huwezi kuzifikia. Kwa hiyo kitu cha kuangalia hapa ni kutunza afya zetu ili ziweze kutusaidia kufikia malengo tuliyojiwekea. Hakikisha unajikinga na magonjwa kwa jinsi unavyoweza na kula chakula kizuri chenye afya.

5. Kuwa na mitizamo chanya.
Hii ndiyo siri kubwa ya mafanikio kwa wajasiriamali wengi. Bila kuwa na mtazamo chanya katika maisha yako halafu ukawa tu unazidi kukomaa kuwa unataka mafanikio hiyo takuwa ni sawa na kujidanganya wewe mwenyewe. Unapojenga mtazamo chanya hakuna kitachokuzuia kuelekea kwenye njia ya mafanikio. Ili kufanikiwa unalazimika kuwa mtu chanya kwanza, ambaye utaona mabadiliko kwako yanawezekana.


6. Kuwa na mahusiano na watu sahihi.
Watu wanaokuzunguka ni muhimu sana katika mafanikio yako. Kama umezungukwa na watu wengi matajiri ni kiwa na maana wenye mafanikio ni rahisi sana kwako kufanikiwa.  Hii yote ni kwa sababu utakuwa unajifunza kwao mambo mengi ambayo yatakufanya na wewe ufanikiwe hivyo hivyo. Ni muhimu sana kukagua marafiki ulionao kama wanakusaidia kukufikisha kwenye ndoto zako au wanakurudisha nyuma?

Hitimisho.

Kwa kufanya mabadiliko hayo utakuwa umejiweka katika nafasi nzuri ya kuweza kufanikiwa zaidi kattika maisha yako. Na ni mabadiliko ambayo yataweza kukutoa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.

Ansante kwa kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO na endelea kuwashirikisha wengine kuweza kujifunza zaidi.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,
dirayamafanikio@gmail.com.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.