google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 11, 2016

Acha Kuupuza Kutumia Mlango Huu Kukufanikisha.

No comments :
Kwa muda mrefu imekuwa ikiaminika kwamba binadamu ana milango mitano ya fahamu. Yaani kuona, kugusa, kuonja, kusikia na kunusa. Hata hivyo, ukweli umebainika kuwa, binadamu ana zaidi ya hiyo milango mitano. Imebainika kuwa, sasa binadamu ana milango sita ya fahamu.
Hii ni moja ya tafiti muhimu kubwa ambazo zimedi kufanywa na wataalamu siku za hivi karibuni. Watafiti hawa wanasema na ili binadamu huyu aweze kutimiza kusudio la uhai wake hapa duniani, sharti autumie mlango huu wa sita wa fahamu ambao kwa muda mwingi umesahaulika ama kupuuzwa na hivyo kushindwa kutumika ipasavyo.
Mlango huu wa sita wa fahamu ni ule unaohusu nafsi ya binadamu. Kwa maana kwamba, huu ni mlango unaohusiana na haja au tamaa ya asili ya binadamu katika mambo ya kiroho. Mahitaji haya ya kiroho ambayo ni ya asili kwa binadamu huambatana na nafsi yake na kujiimarisha zaidi kwenye moyo wake. Ninaposema ‘moyo’, nina maana ya akili na hisia.
Kama ilivyo kwa milango ile mitano ya fahamu ambayo huwasiliana na kuongoza mwili, ndiyo ilivyo pia kwa hisia hizi za kiroho ambazo kazi yake kuu ni kuilinda na kuunganisha nafsi hiyo na muumba wake (Mungu), kuipa nafsi muongozo wa kiroho wa kiroho na kuunganishwa na nguvu ambazo hutuongoza katika njia zetu na makusudio yetu.

UBUNIFU NI MUHIMU
Ile milango mitano ya fahamu hutufanya tuweze kuendelea kuishi juu ya ardhi ya dunia. Lakini mlango huu wa sita au mtikisiko wa ndani kabisa wa kihisia hutupatia mabawa na kutufundisha namna ya kuruka. Hapa ni kwa maana kwamba, hutuongezea uwezo na nguvu za kutimiza ndoto zetu. Ni watu wachache sana wanaotambua ukweli huo na wanaojua kuutumia mlango huo.
Kutokana na jinsi dunia yetu hii inavyozidi kusonga mbele, suala la kuutumia mlango huu halitakuwa suala la hiari tena, bali litakuwa ni suala  la lazima kwa mtu yeyote yule anayetaka kuishi maisha yenye kusudi, salama na usawaziko. Hatupaswi kamwe kuukana uwezo wetu ambao hutupatia hekima na maarifa ya hali ya juu na kuendelea kukumbatia nadharia za kisayansi peke yake.
Ukweli ni kwamba, tuna uwezo mkubwa usiothimilika ndani ya nafsi zetu kuliko vile tunavyoelewa au kwa vile tulivyofundishwa kuamini. Ni jambo la msingi kujifunza kuamini mitikisiko ya kihisia iliyomo ndani mwetu, mitikisiko yenye nishati kubwa sana inayotokana na mlango huu wa sita wa fahamu. Nishati ambayo inatikisika kupitia hali yetu ya kujitambua na kutuongoza kwenye safari ya nafsi, katika maisha kwa ujumla.
Hivyo basi mlango huu wa sita kwa binadamu unahusu umuhimu kwa binadamu kuzingatia masuala ya kiroho ambayo ndiyo yanayoigusa moja kwa moja nafsi yake na kuipatia nishati inayohitajika kwa ajili ya kuendelea kudumu hapa duniani na kutimiza yale yote iliyopangiwa kuyatimiza.
Kupuuza ukweli na umuhimu wa jambo hili ndiko kunakowafanya binadamu waendelee kutesana, kuumizana na hata kuuana. Vilevile faida nyingine inayotokana na kuutambua na kuutumia mlango huu, ni ile inayomfanya binadamu autambue kweli kwamba, binadamu katika ujumla wao ni kitu kimoja na wanategemeana kwa kila hali.
Hivyo, basi lolote unalomfanyia mwingine ni sawa na kujifanyia mwenzako ni sawa na kujifanyia wewe mwenyewe. Kwa hiyo tunapoamini kuhusu mtikisiko huu uliomo ndani mwetu, ndipo tunaweza kusawazisha hali na kuwa na amani ndani mwetu.
Nikutakie maisha mema na endelea kuwashirikisha wengine kuweza kujifunza kupitia mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kila wakati.

Ni wako rafiki katika mafanikio,
Kama una maswali, changamoto au unahitaji ushauri wa kibiashara, usisite kuwasiliana nasi kwa:-
Simu0713 048 035,
E-mail; dirayamafanikio@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.