google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 19, 2016

Faida Kubwa Za Nidhamu Binafsi Katika Kuyafikia Mafanikio Yako Makubwa.

No comments :
Nidhamu maana yake ni utaratibu au sheria anayojiwekea mtu au kuwekewa mtu katika kufanya au kutofanya kitu ama jambo fulani katika maisha.

Mara nyingi nidhamu humwongoza mtu na kumwekea mipaka kwa baadhi ya vitu kuvifanya au kutokuvifanya ima kwa kupenda au kutopenda.

Nidhamu ziko za aina mbili  nidhamu binafsi anayojiwekea mtu binafsi kwa makusudi ya kutimiza malengo fulani aliyojiwekea katika maisha yake. Na kuna nidhamu inayowekwa na kikundi, taasisi, kampuni au serikali ya nchi kwa madhumuni maalumu.

Leo tunaangalia zaidi katika nidhamu binafsi. Nidhamu binafsi ndio imekufanya wewe uwepo hapo ulipo na uwe hivyo ulivyo. Ni kutokana na nidhamu binafsi ndiyo  imekufanya ufanikiwe au usifanikiwe katika maisha yako. Nidhamu binafsi ndiyo inayomwongoza mtu katika kufanya maamuzi sahihi au yasiyo sahihi katika maisha yake.

Zifuatazo ni faida za mtu kuwa na nidhamu binafsi;-

 1. Nidhamu binafasi humfanya mtu kujitambua yuko wapi, ni nini wajibu wake katika maisha yake na jamii inayomzunguka.

2. Humwongoza mtu katika kufanya maamuzi sahihi katika maisha yake kwani humfanya atafakari kwanza hasara na faida ya kile anataka, kabla ya kulifanya.

3. Humfanya atimize malengo yake kirahisi kwa sababu hufikiri kabla ya kufanya mambo.

KUWA NA NIDHAMU BINAFSI.
4. Nidhamu binafsi humfanya mtu kupendwa na watu kwa sababu ya kufanya vitu sahihi na mwenye uhakika navyo.

5. Humfanya mtu asikurupuke na kuiga vitu asivyo na uhakika navyo.

6. Humfanya mtu kutimiza majukumu yake kwa wakati.

7. Humfanya mtu kujiamini na kuondokana na hofu katika maisha.

8. Humafanya mtu kuwa na matumizi mazuri ya muda na pesa.

9. Humfanya mtu kufanya vitu kwa malengo na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

10. Humfanya mtu kujituma na kufanya kazi kwa bidii.

Mbali na faida hizo za nidhamu binafsi, Zifuatazo ni hasara za mtu kutokuwa na nidhamu binafsi katika maisha yake.

1. Huishi kwa kufuata Mkumbo hawi na utaratibu ktk maisha yake ni kama bendera fuata upepo.

2.  Mtu ambaye hana nidhamu binafsi anakuwa hana maamuzi sahihi katika maisha yake na kamwe huwezi kumwomba ushauri mtu asiye na nidhamu binafsi atakupoteza

3. Humfanya mtu kutokujiamini na hivyo kuwa na wasiwasi na hofu katika kufanya jambo lolote. Sijui nitaweza nimtafute nani anishauri ili nisikosee.

4. Humfanya mtu kutumia vibaya muda wake na pesa zake kwani hutumia bila umiliki wowote ule.

5. Ni mtu asiye na malengo huishi kwa kubahatisha na kudra za Mungu. Anasema tutafika tu, ipo sikunami nitafanikiwa tu Siku na miaka inaisha hadi kifo kinamfika hakuna alichofanya.

6. Humfanya mtu kuvunjika moyo haraka pindi anapoanguka au kutifanikiwa katika jambo analofanya. 

7. Humfanya mtu kutokuwa na msukumo wa ndani katika kile anachofanya katika maisha yake hufanya ilimradi tu amefanya bila malengo yeyote.

8. Hukushelewesha au kukunyima kabisa fursa ya mafanikio na kutimiza ndoto zako katika maisha.

9. Ni rahisi kubadilisha maamuzi uliyojipangia na kuanza kufanya kitu kingine ambacho hukukipanga kukifanya.

10. Kukosa nidhamu binafsi humfanya mtu kudharaulika na jamii inayomzunguka kwa kukosa busara na ueledi katika kusema kwake, kutembea kwake na hata kutenda kwake.

Ansante kwa kufatilia makala haya na endelea kuwaalika wengine waweze kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO.

Ni wako katika kupeana hamasa ya kuyafikia mafanikio na uhuru wa kipesa.

Shariff H. Kisuda alimaarufu mzee wa Nyundo Kali. 
 
Simu; 0715079993.
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.