google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 26, 2016

Ndoa Imara Huweza Kutibu Hata Kansa.

No comments :
Maradhi ya kansa yamekuwa yakiwasumbua watu wengi sana kwa nyakati za hivi karibuni. Hata hivyo kuna aina nyingi za kansa, mojawapo ni ile ya kibofu cha mkojo.
Kulingana na utafiti mmoja uliofanywa nchini marekani, imeonesha kwamba, msaada wa karibu unaotolewa na wanandoa kwa wanandoa wenzao ambao, wameathirika na gonjwa wa kansa  ya kibofu cha mkojo, ni aina mojawapo ya tiba inayoweza kuwafanya wagonjwa hao wajisikie vizuri na kuishi kwa muda mrefu.
Utafiti huo ulionyesha kwamba, watu wanaougua ugonjwa huo ambao wako kwenye ndoa, wana nafasi kubwa ya kuishi muda mrefu zaidi ukilinganisha na wenzao ambao hawajaoa au kuolewa. Hali hii haichagui umri, rangi au hata kiwango cha athari ya ugonjwwa wenyewe.
Vilevile, tafiti mbalimbali za huko nyuma ziliwahi kuonesha kwamba, ndoa bora na imara zina uwezo wa kuwaongezea ahueni wanandoa wanaougua maradhi ya kansa ya matiti na ile ya mkojo.

NDOA IMARA INATIBU MARADHI MENGI.
Watafiti hao walizidi kusema kwamba utafiti huo mpya unaweza ukawa na manufaa zaidi kwa aina nyingine ya kansa. Hali kadhalika utafiti huo ulionesha kwamba,wagonjwa wa kansa ambao walikuwa wamefiwa na wenzi wao wa ndoa na wale waliotengana ama kutalikiana, waliathirika na ugonjwa huo zaidi.
Ingawa umri mkubwa nao ulichangia kwa kiwango kikubwa kwenye hali hiyo, kutokuwa na mpenzi kulionesha wazi kuwa na madhara makubwa.
Sababu hasa, inayoyaofanya kuwa na tofauti hiyo, bado haijaulikani. Hata hivyo, yapo maelezo machache yanayoweza kutolewa  kuhusiana na hali hiyo. Kwa mfano, mume au mke anaweza kumshauri mwenzi wake amwone mapema daktari, wakati dalili za mwanzo kabisa za ugonjwa zinapojitokeza. Na pia anaweza kumshauri mwenzake abadili mwenendo wa tabia zinazoweza kuuongeza madhara yatokanayo na ugonjwa huu kwa mfano, kuacha kuvuta sigara, kwani tabia ya uvutaji wa sifara huzidisha kiwango cha ugonjwa huu.
Na pia msaada wa mume au mke, kwa njia moja au nyingine, huzipa nguvu chembechembe hai za mwili zinazohusika na mfumo mzima wa wa ulinzi. Uchunguzi huo ulionesha kuwa, wagonjwa wa kansa ya matiti waliokuwa wameolewa na ambao walihisi kuwa wana uhusiano mzuri na imara na wenzi wao wa ndoa na kuwa wanapewa kila msaada wanaouhitaji, chembechembe zao hai zinazolinda mwili, zilionekana kufanya kazi kwa kiwango cha juu kabisa na hata ziliweza kuua baadhi ya vijidudu vinavyosababisha ugonjwa huo.
Ndoa bora na imara imekuwa ikitajwa sana kama ni tiba inayoweza kutibu maradhi mengi ikiwemo kansa na pia imekuwa ikielezwa kwamba, huufanya mwili wa binadamu kuwa imara zaidi, watu wenye ndoa za mashaka na vurugu, wanapoingia katika maradhi, wameonekana kudhoofu na pengine kufa haraka, ukilinganisha na wale ambao wako kwenye ndoa imara.
Kwa hiyo hapa utajua, inaposisitizwa kwamba,wanandoa wajenge ukaribu ambao utawezesha ndoa zao kuwa bora na imara, siyo tu kwa sababu ya ya kufurahia mahaba, lakini pia ni kwa sababu ya kunusuru afya ya miili yao. Tafiti nyingi zimekuwa zikionesha kwamba, wanandoa ambao wako kwenye vurugu za kindoa hupata madhara mengi ya kimwili, wanawake wanaelezwa kwamba huathiriwa zaidi na jambo hilo.

Kumbuka huu ni utafiti tu uliofanya na wenzetu. Nikutakie siku njema na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO  kila siku, ili uweze kuboresha na kubadili maisha yako.  
Tupo pamoja,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.