google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 23, 2016

Siri Ya Kufanikiwa Katika Katika Kila Jambo.

No comments :
Haijalishi hapo ulipo unafanya kitu gani, lakini ninachotaka kukwambia hapa leo, tambua ipo siri ya kuweza kukusaidia kufanikiwa kwa asilimia zote mia moja, kwa lile jambo unalolifanya. Watu karibu wote wenye mafanikio makubwa wanaitumia siri hii kuweza kufanikiwa.
Kama watu hawa wenye mafanikio wamekuwa wakiitumia siri hii kuwafanikisha, basi hata wewe unaweza kuitumia siri hii kukufanikisha na kubadili maisha yako kabisa. Pengine umekuwa ukishindwa sana kwenye maisha yako miaka na miaka kwa sababu ndogo tu, ya kushindwa kuijua siri hii na kuitumia. 
Ninachotaka kusema na kukusisitiza ni kwamba kwa malengo yoyote uliyonayo, unao uwezo wa kuyafikia ikiwa tu utaamua kuitumia siri hii ya ushindi kukufanikisha. Kumbuka siku zote hakuna uchawi wala muujiza katika mafanikio. Hata wewe unaweza kufanikiwa kwa kishindo ikiwa utazingatia na kufanyia kazi siri hii.
Usijali sana kwa sehemu ulipo kimaisha kwa sasa. Hiyo itabaki kwako kuwa historia. Angalia mbele nakutumia siri hii kubwa ya mafanikio ambayo unakwenda kujifunza sasa. Siri ambayo unatakiwa ujifunze na kuilewa vizuri ni siri ya kutengeneza tabia za mafanikio.

TENGENEZA TABIA ZA MAFANIKIO.
Hautaweza kufanikiwa ikiwa wewe hutajitengenezea tabia za kuelekea kwenye mafanikio unayoyataka. Mara nyingi miili yetu inapenda sana tuendelee kukaa katika hali tulizozizoea. Sasa mafanikio hayawezi kuja kwa namna hiyo ya mazoea. Ni lazima kuna mambo utatakiwa kuyabadilisha au  kutengeneza tabia za mafanikio.
Jaribu kumuangalia Mohamed Ally katika kipindi chake alichokuwa akishinda mapambano mengi ya masumbwi, asingeweza kufika huko kama asingetumia muda mwingi kufanya mazoezi na kujitengenezea tabia za mafanikio. Kilichomfanya afanikiwe ni kujitengenezea tabia za mafanikio na kuwa mtii. Hiyo ndiyo ilikuwa siri ya mafanikio yake.
Lakini si hivyo tu, hata ukichunguza maisha ya watu waliofanikiwa sana, kikubwa kilichowafanikisha na kuwafikisha walipo ni kule kujitengenezea tabia za mafanikio kila siku. Hapa ndipo mafanikio makubwa yanapoweza kuanzia na sio kinyume chake.
Kuna wakati niliwahi kusoma maandiko ya mwanasaikolojia Julia Kristina Mah, amabapo alikuwa akiongelea thamani ya kutengeneza tabia za kukufanikisha. Alisema moja ya tabia inayowafanya watu washindwe kuafanikiwa ni kule kupenda kufanya mambo kwa kujisikia au kuongozwa na hisia sana.
Aliendelea kusema watu wengi wana tabia ya kufanya mambo kwa kujisikia, kama anaona kachoka kidogo basi hafanyi atasubiri mpaka atakapokuwa sawa, hiyo ni tabia inayowarudisha wengi nyuma. Hivyo, dawa ya kutoka hapo ni kutengeneza tabia za mafanikio na si kusubiri.
Kaa chini na ujiulize ni kitu gani unakitaka katika maisha yako? Ukishakijua kitu hicho tengeneza tabia itakayokusaidia kukufikia kitu hicho. Kwa mfano kama unataka kuwa msomaji mzuri, basi tenga muda wa kujisomea kila siku hata kwa dakika ishirini kwa siku, baada ya muda utafikia lengo lako.
Kwa chochote unachokitaka inawezekana kukipata ikiwa utajitengenezea tabia imara za kukufanikisha. Ikiwa lengo lako ni kutafuta mtaji ni sawa, jiwekee akiba kidogo kidogo kila wakati, utafanikisha lengo lako hilo. Hakuna tena nasema hakuna utakachoshindwa kukifanikisha ikiwa una tabia sahihi za mafanikio.
Ni vyema ukaitambua siri hii ukaitumia kukufanikisha. Kumbuka, tabia ni kitu ambacho hufikirii kukifanya bali kina kuwa kwenye damu. Hivyo ndivyo unavyotakiwa kujitengenezea tabia zako za mafanikio. Bila kuchoka kila siku. Kwa kufanya hivyo utajikuta zile kazi ulizokuwa ukizifanya kwa ugumu zinakuwa rahisi sana kwako na kukupa mafanikio.

Ansante sana kwa kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kila wakati. Endelea kuwaalika wengine waweze kujifunza kupitia makala tunazotoa hapa.
Ni wako rafiki katika kuyasaka mafanikio ya kweli,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.