google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 15, 2016

Hatua 6 Za Kuchukua Ili Uwe TAJIRI.

2 comments :
Hivi umeshawahi kujiuliza kuwa  ipo siku unaweza ukawa na mafanikio makubwa hadi kufikia utajiri? Kama bado hujawahi kuwaza hivi hata siku moja, leo nataka nikupe habari njema kuwa hata wewe unaweza ukawa tajiri leo hii endapo utaamua.
Unashangaa! Ndiyo unaweza. Kwa nini nakwambia unaweza? Sikiliza. Kufikia mafanikio makubwa na hatimaye kuwa tajiri si bahati wala muujiza kama ambavyo wengi wamekuwa wakifikiri sana.  Bali ili uweze kuwa tajiri unahitaji kuwa na maandalizi yakutosha na kuchukua hatua muhimu za kukufikisha huko.
Ikiwa utakubali kufanyia kazi hatua hizo basi ni wazi unaweza kufikia utajiri mkubwa ambao upo mbele yako na unaokusubiri. Sasa bila kupoteza muda, naomba twende pamoja kwenye hatua muhimu ambazo unaweza ukazifuata kila siku na kila wakati hadi kuufikia  UTAJIRI.
1. Tengeneza njia nyingi za kukuingizia kipato.
Hakuna njia ya uhakika ambayo inaweza ikakufikisha kwenye utajiri kinyume na kuwa na vyanzo vingi vya pesa. Huwezi kufanikiwa kama maisha yako yanategemea chanzo kimoja cha pesa. Kwa hakika hii itakuwa ni ndoto na pia ngumu sana kwako.
Kwa kuwa umeshalijua lengo lako kubwa unataka kuwa tajiri, hapo sasa unatakiwa kuweka juhudi zote kwa kutengeneza njia nyingine za kujiingizia kipato chako. Kwa kufanya hivyo utakuwa umejiweka kwenye nafasi kubwa ya kufikia mafanikio makubwa na hatimaye kuwa TAJIRI.

MAFANIKIO NI HATUA KWA HATUA.
2. Jiwekee malengo ya kifedha.
Mbali na kutengeneza njia nyingi za kukuingizia pesa, lakini ni vizuri ikiwa utajiwekea malengo yako ya kifedha. Hapa sio suala la kukusanya pesa tu peke yake, inabidi pia utambue unataka kukusanya pesa kiasi gani baada ya muda fulani.
Unaweza ukaanza kujiwekea malengo haya kwa mwezi na hata mwaka. Na unaweza ukaanza kujiuliza ‘mwaka huu ifikapo disemba ni lazima niwe na kiasi hiki cha pesa’. Na unapokuwa unajiwekea malengo hayo, yanakusaidia kukusukuma kufanya kazi kwa juhudi zote ili ufikie malengo yako ya utajiri kwa haraka.
3. Jifunze kila siku.
Watu matajiri siku zote si wajuaji. Ni watu wa kujifunza. Kwa kuwa umechagua njia ya kukufikisha kwenye utajiri, inabidi ukubali kuwa mpole na kujifunza kila siku. Bila kufanya hivyo utaachwa nyuma sana. Hii ni kwa sababu, kwa sasa tupo kwenye ulimwengu wa habari. Kama huna habari za kukufanikisha ni sawa na huna mafanikio kabisa.
Kama ulikuwa huna utaratibu huu unatakiwa kuunza mara moja. Anza kwa kujisomea vitabu. Sikiliza mafundisho ya mafanikio au huwezi hilo hudhuria semina au jifunze kutoka kwa marafiki zako. Naamini ukijifunza utabadilisha maisha yako sana kuliko unavyodhani na kwenda mbele zaidi.
4. Badili mtazamo wako kuhusu pesa.
Mara nyingi mitazamo tuliyonayo ndiyo ambayo hutufikisha hapo tulipo. Jaribu kuangalia hili kwa undani utagundua ukweli huu. Hata kwenye mambo ya pesa na mafanikio ni hivyo hivyo. Ili uweze kufanikiwa kuna umuhimu wa kubadili sana mitazamo yako kuhusu pesa.
Kila unapoifikiria pesa unakuwa una mtazamo upi? Je, unaiona pesa ni adui? Unaiona pesa kama ni shetani kwako au unaionaje? Kwa vyovyote vile kama una mtazamo hasi kwenye fedha huwezi kuwa tajiri. Ni lazima uione pesa kama rafiki yako wa karibu ili ufanikiwe.
5. Tatua changamoto zinazowakabili watu.
Watu wenye mafanikio siku zote ni watu wa kutatua changamoto zinazowakabili watu. Hawa ni watu ambao huwa si walalamikaji sana, ni watu wa kuchukua hatua dhidi ya maisha yao na ya wengine. Hicho ndicho kitu ambacho huwafanya wapate pesa na  fursa nyingi siku hadi siku.
Kwa jinsi wanavyotatua matatizo ndivyo ambavyo pesa inazidi kumiminika. Hakuna ubishi wala mtu atakayekuzuia kupata pesa ikiwa wewe unatatua changamoto zinazowakabili watu. Ni lazima upate pesa hata iweje. Tena kuna wakati hizo pesa watakuletea wao wenyewe hata kama umelala.
6. Fanya kitu cha  kukutoa kwenye hali ya mazoea.
Kuna wakati ambapo tunakuwa tunaamka hatujisikii kufanya kile tunachokifanya. Hapa sasa ndipo ambapo unatakiwa kufanya hivyo hivyo. Unatakiwa kutoka kwenye mazoea uliyonayo na kujisukuma mpaka kufanya kitu hicho kwa ngvu zote hata kama unajiona huwezi.
Kwa kadri utakavyozoea kujisukuma kufanya mambo nje ya yale uliyozea yaani kutoka kwenye ‘Comfort zone’ kwa mazoea uliyozea, utazidi kujiweka kwenye mafanikio. Kama unaona mambo yako ni magumu jisukume vivyo hivyo kuyafanya hadi kufikia mafanikio makubwa.
Hizo ndizo hatua unaweza kuchukua kwa sasa kufikia utajiri. Jiwekee malengo ya kufikia utajiri wako bila kuacha. Ansante kwa kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kila wakati. Waalike wengine waweze kujifunza kupitia makala tunazotoa hapa.

Ni wako rafiki katika kuyasaka mafanikio ya kweli,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,



2 comments :

Note: Only a member of this blog may post a comment.