google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 29, 2016

Kanuni Ya Usumaku (Law Of Attraction).

No comments :
Na Apolinary Protas wa Jitambue sasa.

Kwa wengine hupenda kuita ni Law of Attraction, lakini kwa upande wangu naona sio lazima niipe jina kwa kuitafsiri moja kwa moja kwenye kiswahili kama ilivyo kwenye kingereza lakini napendelea kuipa jina la Sheria ya Sumaku kwani jina hilo inakuwa rahisi kuielewa vyema. 

Kama inavyofahamika kuwa Sumaku ni kifaa ambacho kinavuta Chuma. Kama una sumaku, ukiiweka karibu na chuma utaona inavuta vitu vyenye asili ya Chuma. Usumaku ni ile hali ya uwezo wa kuwa na nguvu kama za sumaku, uwezo wa kuvuta vitu vyenye hali ya chuma. Je usumaku ni nini?

Kanuni ya Usumaku ni nini?

Ni kanuni inayotazama kuwa Ufahamu wa mwanadamu una sifa ya Sumaku. Kile kilichopo kwenye ufahamu wako unakiumba na kukipelekea kuwepo katika dunia yako. Kila jambo unaloliona halipo kwenye ufahamu wako tu lakini linaweza likawa kwenye ufahamu wa mwingine hivyo lipo kwenye ufahamu (ufahamu fulani). Chukulia ulimwengu kama umeme. Umeme huo upo katika hali mbalimbali ya nguvu na kila hali ina upekee wake. Ufahamu ni umeme, na ndio maana kwenye Ubongo kuna neva, neva hupitisha umeme kutoka kwenye ubongo na kwenda kwenye sehemu nyingine za mwili kama vile msuli na milango ya ufahamu. 

UNA UWEZO WA KUUMBA MAISHA YAKO.
Ufahamu ni kiini kikuu cha Mwanadamu na kila kiumbe. Kila kiumbe kina ufahamu wake kulingana na hali iliyopo lakini mwanadamu ndiye mwenye ufahamu wa kujitambua yeye ni nani. Na kuutambua ufahamu wake, lakini aina nyingine za uhai haziwezi kufahamu ufahamu wake ni nini na umeumbwa na aina gani ya ufahamu. 

Ndani yako kuna sehemu kubwa sana iliyo na nguvu kubwa sana ambayo huijui. Unaweza ukajiuliza ulipokuwa mdogo nani alikuwa anahakikisha unakua vyema, nani anahakikisha sasa hivi mapafu yako yanasukuma hewa, nani anayehakikisha moyo wako unadunda, ni sehemu ambayo unayo akilini mwako lakini tangu uumbwe mpaka leo hujawahi kuitazama na kujifunza kuitawala. Simaanishi ujue kutawala mapigo yako ya mwili bali namaanisha kuwa ndani mwako kuna nguvu kubwa, ambayo ukiamua kuiamuru kufanya chochote inaweza kukusaidia na kukupa chochote. Nguvu hiyo inaungana na ufahamu wako. Unachokiamini, unachokitafakari, na unachokisema kinaungana na nguvu hiyo vyema na kupelekea kufanyika. Unaweza ukawa hujaona hilo lakini ukiwa makini utagundua hilo. 

Kanuni ya USUMAKU inatufunza kuwa, unaumba uhalisia wa maisha yako wewe mwenyewe. Wewe ni kama Sumaku, unavuta uhalisia wowote ule ambao unaushikilia akilini kwa muda mrefu. 

Ukiamini kuwa wewe ni mtesekaji utazidi kuwa mtesekaji, ukiamini umebarikiwa basi unapata baraka, na ukiamini unaweza kutimiza jambo fulani nawe utaweza kulitimia. 
Hata Yesu alisema; Ukiwa na imani kidogo kama vile Punje ya Haradani unaweza kuuamuru mlima kuhama na ukahama. Jitambue Sasa na yatengeneze maisha yako vyema. 

Ansante kwa kusoma makala haya na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kjifunza.




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.