google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 24, 2016

Ijue Elimu Hii Muhimu Ya Fedha Na Mafanikio, Ili Uwe TAJIRI.

No comments :
Leo ngoja tuzungumze juu ya fedha na vitu vinavyoambatana na fedha(Assets au Liabilities) ambavyo ni chanzo kingine cha kupima mafanikio yako au hata kujua utapita njia ipi kufikia malengo yako.

Watu wengi wamedumaa na kushindwa kusonga mbele kwa kukosa maarifa sahihi juu ya neno FEDHA.  Na bahati mbaya ualisia wa somo hili kivitendo halielezwi kisahihi shuleni au vyuoni, hapa naomba usinielewe vibaya na wala usije sema najifanya mjuaji la hasha.

Labda nitoe mfano. Shuleni au vyuoni ukifeli wewe unaambiwa mjinga lakini kwenye usakaji wa fedha uhalisia wa kufeli ni hatua mojawapo kufikia malengo maana ukiogopa kufeli kamwe sahau kuhusu mafanikio, maana hutaweza kujaribu kitu.


Pili shuleni/chuo unafundishwa kila swali lina jibu moja tu sahihi (1+1=2) lakini kwenye uhalisia inawezekana kabisa 1+1=6 na bado likawa jibu sahihi.

Shuleni/vyuoni hauruhusiwi kuigilizia hasa wakati wa mtihani lakini kwenye uhalisia wa kusaka mafanikio kudesa unaruhusiwa-bila shaka umeona kwanini nilipinga hapo juu.

Kuza ufahamu wako wa fedha kila siku.

Elimu ya fedha ni muhimu sana kuijua kwa undani na hapa nisisitize usije ukaridhika kamwe na ‘material’ yako ya darasana na A+ zako halafu ukajiona unaweza ukatoboa kirahisi kwenye uhalisia, hizo zilikuwa nadharia tu, vitendo ndiyo mpango mzima.

Hakikisha unasaka elimu zaidi juu ya fedha na matumizi yake sahihi. Huwa nasikitika sana kumwona kijana kwanza amepata kazi na kitu cha kwanza anachowaza ni gari!! Eti kwa kuwa ana kamshahara kaa milioni moja na laki mbili.

Kijana huyu anakuwa anajisahau kuwa amechimba shimo la kuchoma pesa hata kabla hajaimalika kifedha. Gari, nyumba unayomiliki, flat screen, radio, smart phone na vinginevyo hizo ni ‘liabilities’ ambazo zitaendelea kukumalizia kamshahara kako na kukufanya usimame pale ulipo kwa miaka mingi.

Kuwa makini, ishi maisha ambayo yanaendana na malengo yako. Kidogo ulichonacho kina thamani kubwa kama utakitumia vizuri, acha kuishi ili watu wakuone ishi wewe na usiishi wao!!

Nunua ‘asset’ maana zitakufanya uzalishe fedha na si kukimbilia kununua mchwa wa kutafuna hata kile kidogo ulicho nacho! Mfano wewe unakimbilia kununua viti vya kutembelea na mwenzako akanunua bodaboda ya kuzungusha machoni pa wengi wewe wa viti  vyako utaonekana mjanja lakini kiuhalisia mwenye bodaboda ni bora mara 1000 zaidi yako!

Hebu nikuambie kitu leo, acha uoga wa kuanza kidogo kwa kamtaji kidogo ukidhani si chochote, na ukasubiria hadi upate mamilioni ndiyo uanze safari yako ya mafanikio.

Utakuwa unajidanganya maana njia ya mafanikio iliyobora na matajili wengi wameitumia ni kuanza kidogo lakini kuwa na malengo makubwa. Na hiyo inasaidia sana kuendelea kujifunza kadili unavyokua (Nyani mzee amekwepa mishale mingi).

Hata Dangote tajili wa Afrika anakushauri (start small dream big). Cha msingi hakikisha unajifunza kuhusu pesa kila iitwayo siku kupitia vitabu, machapisho, semina za ujasiliamali au warsha mbalimbali (Kama kweli unataka kubadilika lazima uwekeze huko). 


Jifunze kuwa mpya kila siku/mwaka kwa kuongeza marafiki wapya hasa wale ambao wanafanya vizuri katika nyanja unazopenda! Na si dhambi kuachana na marafiki ambao wanakukatisha tamaa kila uchwao.

Hamna lisilowezekana chini ya jua kama utakuwa na imani ya kumtumaini Mungu na kuamini ana mpango na uwepo wako hapa dunia. Fanya kwa moyo bila chembe ya shaka hakika utafika.

Waliofanikiwa wengi ukiwauliza walifikaje walipo watakuambia kwa kweli hawajui ila wanachojua walifanya kazi kwa moyo na imani kubwa kuelekea kwenye malengo yao na Mungu atimaye amewawezesha.

Sasa kwanini wewe usite!!? Kuwa mdadisi na mwenye kiu halisi ya kile ukitakacho hata kama kijiji/mtaa mzima watakucheka kuwa hutaweza wewe jisemee tena ukijiamini kuwa unaweza kwani Mungu akiwa upande wako hakuna linalo shindikana!!

Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

MAKALA HII IMEANDIKWA NA SHARIFF KISUDA alimaarufu mzee wa nyundo.
Mawasiliano 0715 079 993

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.