google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 21, 2016

Acha Kurudia Kufanya Kosa Hili, Wakati Unatafuta Mafanikio.

No comments :
Kati ya kitu muhimu sana ambacho kinaweza kukusaidia katika safari ya kuelekea mafanikio yako, ni yale makosa unayoyafanya. Mara nyingi makosa hayo ukiyatumia vizuri ni nguzo kubwa ya kukusaidia kufanikiwa.
Lakini pamoja na makosa hayo kuwa ni msingi wa kukufikisha kwenye mafanikio, naomba ieleweke kwamba si makosa yote, yanaweza kukusaidia kufanikiwa. Yapo makosa ambayo hutakiwi kurudia kuyafanya kwenye maisha yako kabisa.
Ikiwa utakuwa ni mtu wa kurudia rudia kufanya makosa hayo mara kwa mara ni lazima safari yako ya mafanikio itakwama. Moja ya kosa kubwa ambalo hulitakiwi kulifanya tena katika maisha yako ni kosa la kutokuchukua hatua ndogo ndogo.
Acha kufanya kosa la kutokuchukua hatua ndogo ndogo kwenye maisha yako. Hatua hizi ndogo ni muhimu sana katika kukufikisha wewe katika mafanikio makubwa, ingawa unaweza kaziona hazina maana.
Kila hatua ni mafanikio.
Wakati wote acha kabisa kujijengea dharau kwamba, hatua ndogo haziwezi kukufikisha popote, kwa chochote kile kidogo ulichonacho usikione eti hakiwezi kukusaidia katika safari yako ya mafanikio, hicho kina msaada mkubwa sana kuliko unavyofikiri.
Kwa mfano, kama unaona una muda kidogo, tumia muda huo kidogo kufanya jambo la maana, hata kujisomea ila usiupoteze. Kama unaona una pesa kidogo, hata kama ni shilingi elfu moja, iweke pesa hiyo na usiipoteze eti kwa sababu ni ndogo.
Pia kama unaona una mtaji kidogo, tumia mtaji huo uweze kuwekeza na kukusaidia kutoka hatua moja na kuelekea hatua nyingine. Chochote kile kidogo ulichonacho, chukua hatua ya kukitumia kwa manufaa ili uweze kufanikiwa.
Utapoteza fursa nyingi na mafanikio makubwa kwa sababu ya tabia ya kudharau mambo madogo. Pengine tu, naomba nikukumbushe mafanikio yanajengwa na kanuni au vitu vidogo vidogo sana ambavyo wengi wanavidharau na kuviona havina msaada kwao.
Unachotakiwa kuelewa ni kwamba kila wakati kwa wewe kuwa makini na kutambua mchango wa mambo madogo madogo katika suala zima la kukufanikisha. Ikiwa utaendeleza dharau au tabia ya kutokuzingatia mambo madogo na kuona hayafai, nakupa uhakika huwezi kufika mbali kimafanikio.
Jenga mafanikio yako leo kwa kuchukua hatua ndogo sana hata kama zinaitwa hatua za kutambaa. Hivyo ndivyo mafanikio makubwa yanavyoanza, yanaanza kidogo kidogo sana.
Najua ni shahidi mzuri wa hili, ukiangalia makuzi ya mtoto, baadhi ya miti mikubwa kama mibuyu, ilianza kidogo kidogo sana, lakini leo hii ukuaji wake ni mkubwa sana ambao hauna mfano.
Tafakari juu ya hili na chukua hatua za kufanya chochote kile hata kama ni kidogo, lakini tambua kina msaada mkubwa sana kwa mafanikio yako leo na kesho, isitoshe naweza kusema huo ndio msingi mkubwa wa kimafanikio unavyojengwa duniani kote.
Dira ya mafanikio inakutakia siku njema na mafanikio makubwa yawe upande wako.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku na pia endelea kuwashirikisha wengine makala nzuri zinazotolewa hapa.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.