google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 30, 2016

Sifa Kuu Za Mjasiliamali Ndizo Hizi.

No comments :
Naamini katika kujifunza, hii ndiyo kauli yangu ambayo inaongoza maisha yangu kila wakati. Kama na wewe unaamini katika kujifunza nakusihi twende sawa.

Somo letu la leo nililipenda sana, na nikaona na niweze kukushirikisha katika somo hili,  somo hili alinifindisha mwalimu wangu wa saikolojia, mtoa siri za mafanikio, au huwa napenda sana kumuita mzee wa nyundo kali huyu si mwingine ni Sharrif Kisuda.

Ambapo katika somo hilo alinifundisha kiundani kuhusu maana halisi ya mjasilimali. Mwalimu wangu huyu alianza kunieleza kwa kusema  maana ya
Ujasiliamali.

"Watu wengi tunapenda kutumia  jina hili la ujasiriamali  lakini wengi wetu hatujui maana yake.”  Aliendelea kueleza ya kwamba Ujasiriamali ni Fursa ya mafanikio ambayo mtu yeyote bila kujali elimu yake au hali yake anaweza kuanzisha biashara au mradi wowote mkubwa au mdogo na kumwingizia kipato bila kutumia nguvu kubwa hatimaye kupata faida.


Watu wengi pia tunashindwa kutofautisha kati ya mfanyabiashara na mjasiriamali. Hawa ni watu wawili tofauti kabisa.  Mjasiriamali ni mbunifu au mtoa wazo la Bbiashara linaloweza kuzalisha Bidhaa. Lakini mfanyabiashara ni mtu anaye uza bidhaa iliyokwisha zalishwa na mjasiriamali kwa lengo la kupata faida. Hapo ndipo utapogungua mfanyabiashara ni mtumwa wa mjasiriamali. 

Japokuwa wote wanategemeana ili mmoja asipokuwepo mwingine anaweza kupoteza kabisa mwelekeo wake. Kwahiyo mjasilimali lazima ashirikiane na mfanyabiashara  katika kutimiza lengo mahususi la muhusika.

Na kila wakati lazima utambue ya kwamba Ujasiriamali una kanuni ambazo unapaswa kuzijua ili kutengeneza au kuzalisha Kitu chenye ubora,  ila katika Biashara haina kanuni ni kuangalia uhitaji wa soko na idadi ya Wateja. 

Kuwa mjasiriamali sio lazima usome mpaka upate digrii ya ujasiriamali zaidi unahitaji kusoma na kuzingatia taratibu na kanuni sahihi. Msingi wa awali wa Mjasiriamali ni wazo lakini msingi wa kwanza wa mfanyabiashara ni Pesa ya mtaji.

Kila Mjasiriamali ni mfanyabiashara lakini si kila mfanyabiashara ni mjasiriamali. Mjasiriamali ni mtu mwenye imani katika kila jambo analofanya na pia mtu aliyetayari kufanya maamuzi bila ya kujali sana matokeo. 

Mjasiriamali ana tabia ya kufanya Kitu anachokipenda na ndio maana huwa vigumu kukata tamaa hata kama kukitokea changamoto kiasi gani. Ni mtu jasiri na anaethubutu kufanya vitu ambavyo wengine huviogopa kuvifanya.

Na zaidi mjasiriamali ana nidhamu ya hali ya juu katika matumizi ya muda pesa na mali zake. Tofauti na mfanyabiashara akipata pesa ya ziada ni lazima aongeze matumizi na starehe zisizo na ulazima.

 Ngoja tuangalie sifa za mjasiliamali.

1.Hufanya kazi kwa bidii.

Mara kadhaa hauna haja budi kuchukia kuwepo katika ulimwengu huu eti kwa sababu Maisha ni magumu, ugumu wa maisha una sababishwa na wewe mwenyewe.

Na hii yote inatokana na kuweza kufanya kazi kimazoe, Mara nyingi ukiwa na tabia ya kufanya kazi kimazoea hata kwa kile kidogo unachokifanya hautakiona thamani yake. Hivyo nakusihi kila wakati hakikisha unafanya kazi kwa bidii huku ukiondokana na dhana ya ya kufanya kazi kimazoea.

2. Lazima awe mbunifu na mvumbuzi.

Hii ni tabia kubwa muhimu ambayo kwa kila mjasiliamali yeyote yule lazima awe nayo, bila ubunifu kwa hicho unachokifanya Ni bure. Ubunifu si kutengeneza kitu awali/ au Ni kitendo cha kufanya maboresho.

Kwa mfano utaona kila siku kampuni fulani za utengenezaji simu, kila kukicha wanafanya ubunifu kwenye bidhaa zao, hufanya hivyo ili kuongeza wateja. Kama ilivyo katika utengenezaji wa simu tumia kanununi hiyo hiyo katika kuboresha vitu ambavyo unavitengeneza au kuvifanya. 

3. Yupo tayari kujifunza kila wakati.

Kama nilivyoeleza hapo awali ya kwamba ujasiriamali ni imani, hivyo mara kadhaa kuamini ya kwamba mafanikio yanakuja kwa kujifunza vitu ambavyo vitamfanya aweze kukua kwa kile akifanyacho. Na vilevile yupo tayari kwa chochote ambacho huwa anafanya.

Ukitaka kuwa mjasilimali wa kweli, hakikisha ya kwamba unayazingatia hayo, kwa umakini zaidi na kuyafanyia kazi.

Imeandikwa na Afisa mipango Benson Chonya.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.