google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

May 17, 2018

Ili Ufanikiwe, Maisha Hayataki Wewe Uwe Na Kitu Hiki…

No comments :
Kama una lengo la kujiongezea kipato, acha kuogopa kufanya kitu chochote. Kama kuna kitu fulani ambacho unatakiwa ukiuze, hebu uza kitu hicho. Acha kujisikia vibaya kwa sababu unauza kitu fulani eti ambacho hakina hadhi yako.
Maisha hayataki aibu, fanya kitu chochote cha kukukiingizia kipato ilimradi kitu hicho kiwe halali na hakiwaumizi wengine. Maisha ya kuona aibu kufanya jambo fulani yatakufanya uzidi kukosa pesa kila kukicha.
 Acha kuwa na ndoto za kufanya mambo makubwa saana na halafu ukadharau kufanya hata vidogo ambavyo huna. Kumbuka, jiwekee ndoto kubwa sana lakini anza na hapo ulipo, anza na kidogo ulichonacho pasipo kujali ni kitu gani.
Hutaki kufanya kitu kwa sababu ya kuona aibu, jiandae kufikia ndoto zako hutaweza kufanikiwa. Kwa nini uone aibu kwa kile ambacho kinakupatia kipato? Shida yako iko wapi na hapo unatakiwa ujiulize.

Ukiona unaona aibu kwa kile unachotaka kukifanya ujue kabisa hujaamua kujitoa kabisa kuweza kufanikiwa. Huna sababu ya kuendelea kuona aibu, ni ukweli uliowazi wewe hapo huna kitu, sasa aibu ya nini?
Inawezekana zipo sababu ambazo zinakufanya uone aibu, sanasana pengine labda umesoma kwa hiyo unaona ukiweka genge mtaani kwako unakuwa ni mtu kama wa kujizalilisha yaani genge sio hadhi yako.
Naweza nikakubalia sawa, sasa kipi unachoweza kufanya ambacho ni hadhi yako? hapo ulipo najua unaweza ukawa una tai vizuri lakini unashindwa kutatua tatizo la shilingi elfu mbili tu, lakini na tai yako shingoni. Sasa kwa hali hiyo aibu ya nini?
Hapo yaani inaonyesha unashindwa kutatua tatizo dogo la shilingi elfu mbili na usomi wako. Jiulize tu mwenyewe je, ni akili kweli kuona aibu kufanya kitu cha faida yako? Kipi bora uendelee kulala au uzunguke mtaani na kuamua kufanya  kitu cha faida.
Nikwambie tu, kwa sasa nyakati zimebadilika sana, kuendelea kujishaua wakati maisha yanataka uyabadilishe huwezi kufanikiwa. Kama unaendelea kupaka rangi kwenye maisha yako, nakwambia endelea kupaka rangi, kuna watu wanajenga ujue na hawapaki rangi.
Mambo hayakusubiri ili yabadilike, ila wewe ndio unatakiwa kuyabadilisha mambo hayo hatua kwa hatua. Huhitaji kufanya kitu maalumu sana ili ufanikiwe, anza na kitu chochote tu, ambacho kinakuingizia kipato bila kujali ni nini, ila kiwe halali.
Acha kusikiliza maneno ya watu, funga masikio na kuamua kufanya jambo lolote mahali popote na eneo lolote, ilimradi jambo hilo liwe ni la kukuingizia kipato. Tafakari kwa kina na fanya uamuzi wa busara wa kuacha kuona aibu zisizo na msingi.

Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.