google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 22, 2015

Kama Hujui, Hawa Ndiyo Watoto Wenye Akili Nyingi zaidi.

No comments :
Hivi karibuni kumekuwa na maneno hata mijadala kuhusu watoto wanaozaliwa kwa njia ya upasuaji. Kuna madai na maneno kwamba, watoto wanaozaliwa kwa upasuaji wanakuwa na akili kubwa sana ukilinganisha na wenzao wanaozaliwa kwa njia ya kawaida.
Wataalamu wa sayansi ya utabibu hivi sasa wanakiri kwamba, watoto wanaozaliwa kwa njia ya upasuaji, wanakuwa salama kiakili kuliko wale wanaozaliwa kupitia njia ya kawaida.
Karibu watoto watatu kati ya kila kumi, wanaozaliwa kwa njia ya kawaida, huwa wanapata tatizo la kuvuja damu ubongoni, ambalo husababishwa na mchakato mzima wa kujifungua kwa mama.
Hivi sasa bila shaka, unaweza ukajua ni kwa nini watu wanaamini kwamba, watoto wanaozaliwa kwa upasuaji wanakuwa na akili kuliko wale wanaozaliwa kwa njia ya kawaida. Kama ulikuwa hujasikia, inabidi ujue kwamba, imani hiyo imeingia na inakua haraka.
Kuna kipindi ambapo wataalamu wa chuo cha utabibu cha North Carolina, waliwahi kusema kwamba, watoto wanaozaliwa kwa upasuaji, wanakuwa na akili salama zaidi.

Waliweza kukiri pia kwamba, kuna uwezekano kuwa, uzaliwaji kwa njia ya kawaida, huathiri kwa kiasi fulani ubongo wa mtoto. Kwa wale watatu katika kumi athari huwa kubwa zaidi.
Kwa wanaozaliwa kwa njia upasuaji, hakuna hata mmoja anayeweza kupata athari ya kwenye ubongo. Ndiyo maana wale wanaozaliwa kwa njia hii, inatabiriwa kwamba, wanaweza kuwa na akili kubwa au salama.
Hata hivyo, watafiti hawa wanasema, ugunduzi huu hauna maana ya kuwataka akina mama kung’ang’ania kujifungua kwa njia ya upasuajii ili kuwafanya watoto wao kuwa na akili nzuri na salama.
Mtoto anapozaliwa kupitia kwa njia ya kawaida, huwa anatoka damu kidogo ubongoni, lakini wataalamu wanajipa moyo kwamba, huenda hiyo ni njia ya maumbile katika suala zima la kujifungua.
Hivi karibuni ndipo ambapo imebainika kwamba, katika harakati za kujifungua kwa njia ya kawaida, kichwa cha mtoto huwa kinabanwa na ubongo kupata msukomsuko.
Jambo kama hili halitokei kwenye kujifungua kwa njia ya upasuaji, kwani hapo hakibanwi na chochote.
Dk. Honor Wolfe, wa chuo hicho anakiri kwamba, watoto wanazaliwa kwa njia ya upasuaji wana uhakika wa kuwa na ubongo usio na kasoro, ukilinganisha na wale wanaozaliwa kwa njia ya kawaida.
Maana yake ni kwamba, kujifungua kwa njia ya upasuaji inaweza ikaanza kuwa ‘fasheni’ kwa siku za karibuni.
Ni wazi akina mama wengi wangependa kuona wanazaa watoto ambao wako salama kiakili kadri inavyowezekana.
Kuna watu wanaosema kwamba, utafiti huo hauna jipya , kwani binadamu amekuwa akizaliwa kwa njia ya kwaida kwa miaka nenda rudi.
Kama ni hatari, basi ilitakiwa iwepo, kwani upasuaji ni njia inayotumika kama kuzaa kwa kawaida kumeshindikana.
Lakini, bado ukweli upo kwamba, huenda wengi watu tumeathirika kiakili wakati wa kuzaliwa. Kama tumeathirika kiakili wakati wa kuzaliwa haina maana kwamba, ni lazima liwe jambo la awaida.
Kama kila watu kumi unaokutana nao, watatu walivuja damu ubongoni wakati wa kuzaliwa , hatuwezi kusema ni jambo la lazima au kimaumbile.
Jarida la Radiology linaonesha kwamba, watoto wanaozaliwa Marekani kila mwaka, kwa mfano kati ya milioni 4, milioni 1.1 huzaliwa kwa upasuaji.
Idadi hiyo imeongezeka hivi karibuni kwa kadri wazai wanavyoamini kuhusu utafiti huu. kwa afrika kujifungua kwa upasuaji hakuko kwa kiwango kikubwa.
Nilichotaka kusema hapa ni kwamba ni kweli wale watoto wanaozaliwa kwa upasuaji wanakuwa na akili kubwa au iliyo na usalama zaidi.
Tunakutakia mafanikio mema, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika.
Ni wako rafiki katika mafanikio,         
Imani ngwangwalu,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nasi kwa:-
Simu;  0713 048 035,                               
E-mail; dirayamafanikio@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.