google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 20, 2015

Kama Unataka Kutimiza Ndoto Zako, Acha Kufanya Makosa Haya.

No comments :
Kila mmoja ana ndoto zake katika maisha, kila mmoja ana njia yake ambayo anaiamini inaweza kumsaidia katika kutimiza ndoto zake za maisha. Ndoto ni kama malengo ambayo kila mmoja anakuwa amejiwekea katika safari yake ya maisha. Mafanikio ni pale unapokuwa umeweza kutimiza ndoto zako. Kuna ambao walishindwa kutimiza ndoto zao labda kutokana na kutoelewa mambo machache ambayo walioweza kutimiza mipango yao waliweza kuyaelewa.

Je unaweza kuiweka ndoto yako kuwa hai? Kuweka ndoto hako hai na kuiishi ni kuepuka kufanya makosa ambayo wengi waliokata tamaa walishindwa. Je ni makosa gani ambayo wengine hushindwa na kupelekea ndoto zao kuzimika?

1.Wasiwasi.
Wapo ambao ndoto zao zimezimika kwani wamekuwa na wasiwasi sana. Unaweza ukawa unajiuliza "Je nitafanikisha kweli?". Wasiwasi hauna nguvu yoyote katika kupelekea mambo yaende sawa bali huaribu mambo kwenda sawa. Wasiwasi hukatisha tamaa, na kupelekea mtu kuona kuwa hawezi kutimiza malengo yake. Una wasiwasi wa nini? Unapoona una wasiwasi chekelea na uuambie wasiwasi wako kuwa "Nitazidi kuwa imara". 

Woga ni kitu ambacho kinatenganisha watu waliofanikiwa na waliofeli kufanikiwa. Kumbuka maana ya kufanikiwa simaanishi pesa na umaarufu bali hali ya kuweza kutimiza malengo yako uliyopanga ni mafanikio pia. 

Hivyo badala ya kuruhusu wasiwasi ukutawale, endelea kuweka msimamo na kushikilia malengo yako.
kweli
MIPANGO MIZURI YA MALENGO NI MUHIMU KUJIWEKEA.
2. Usikubali vikwazo vikutawale.
Kwa kifupi ni kuwa lazima utakutana na vikwazo, vikwazo ni jambo la kawaida katika maisha, vikwazo vipo kwa lengo la kutuimarisha. Na kama kungekuwa hamna vikwazo tusingeimarika kwani kujisahau kungeongezeka. Vikwazo vinatakiwa uvitazame kama vile ni ngazi, vinakusaidia kupanda hali fulani na tunapaswa kujifunza na kuwa imara zaidi katika hali za vikwazo. 

Ukifuatilia watu walioweza kuishi katika ndoto zao kila mmoja atakuambia ni lini alipopata kikwazo kikuu ambacho hatasahau, wengine walikataliwa kuwa hawawezi, wengine walikosa hata uwezo wa kutimiza ndoto zao, lakini wote hao ambao wamefanikiwa japokuwa walikutana na vikwazo hivyo, watakuambia kuwa HAWAKUKATA TAMAA. 

Hawakuruhusu vikwazo viwatawale na kuwarudisha nyuma. Walizidi kuimarika na kusonga mbele na kuzidi kushikilia nia yao.

3. Kubaliana na hali uliyonayo.
Hali uliyonayo hivi sasa inabadilika. Maisha hubadilika na hayabaki sawa milele. Hali zinapita, utazidi kukutana na watu mbalimbali, utazidi kujifunza vitu mbalimbali na maisha hayataacha kukundisha. Wapo ambao wamekata tamaa kutokana na hali waliyonao hivi sasa haiwezi kuwafikisha pale wanapodhamiria lakini wanasahau kuwa mambo hubadilika. Jambo dogo linaweza kubadilisha maisha yako yote na hukutegemea. Maisha ni maajabu. 

Kubali hali ya sasa na maisha yako ya wakati huu, shukuru kwa uhai ulio nao, marafiki wanaokuelewa, na tafuta kitu cha kushukuru nacho badala ya kujiumiza kwa mawazo na lawama. 

Kubali wakati huu wa sasa, shukuru kwa kila jambo, huku ukifanya juhudi kuhakikisha unaendeleza malengo yako. Hata kwa madogo shukuru.

4. Kushikilia yaliyopita.
Kosa lingine ambalo wengi hukosea na mwishowe kushindwa kutimiza malengo yao ni kushikilia wakati uliopita. Bado wanaishi kwa kuwaza makosa waliyoyafanya, mazuri waliyopoteza n.k. Wakati uliopita ulishapita, wakati uliopo ndio wakati ambao unakupa nafasi wewe kujirekebisha na kuishi vyema. Wakati ujao nao unategemea wakati huu wa sasa kutabirika. Kama wakati huu wa sasa unautumia vyema na kuweka malengo utasonga mbele. 

Kumbuka hakuna kiasi cha majuto ya wakati uliopita kinachoweza kubadili yaliyopita na hakuna kiasi cha wasiwasi kuhusu wakati ujao ambacho kinaweza kuubadili wakati ujao bali wakati huu wa sasa ndio pekee kwetu sisi. Jifunze kwa yaliyopita na zidi kusonga mbele.

 5. Kusahau kujitunza.
Wengine husahau hata kutunza miili yao, kula kwa afya, mazoezi, na kuhakikisha wana afya ya mwili, akili na roho. 
Huwezi kufurahia matimizo ya ndoto zako kama una afya mbaya, kama umezungukwa na tatizo. Usikubali kupoteza uhai, kuharibu afya yako, au kufanya ambacho kinaashiria huwezi kujitunza na kujithamini. Unapaswa kujijali na kutambua kuwa nawe unastahidi kujijali badala ya kujali ndoto/malengo yako tu.

TAFUTA MSAADA IKIWEZEKANA
6. Kusubiri msaada ukusaidie.
Wapo ambao wanaamini bila kusaidiwa hawawezi kutimiza ndoto zako. 
Labda nitoe mfano mzuri, unaweza siku moja ukakutana na mtu na kutokana na kujitambua kwako ukaweza kuweka urafiki mzuri na mtu yule. Kumbe mtu yule anafahamiana na fulani ambaye naye kuna kitu ulichokuwa unahitaji sana kusaidiwa na anakuunganisha na mwishowe unajikuta umepata mtu wa kukusaidia kutimiza ndoto zako. 

Sio kwamba hali ya kusaidiwa haitokei bali hutokea, kumbuka Mungu hana mikono kwamba itashuka mikono mawinguni na kukupa unachotaka bali ulimwengu ukitaka kukupa kitu fulani au huduma fulani hutumia wanadamu wenzio kukufunza na kukusaidia. Badala ya kutegemea msaada bali endelea kuishi vyema, heshimu kila mmoja awe wa chini yako au wa juu yako. Ishi na watu vyema na ishi katika haki. Haimaanishi ukifanya hivi itakusaidia moja kwa moja bali itasaidia njia yako ya kutimiza ndoto zako kwa kukuweka katika amani na watu. 

Wengine husubiria mpaka wawe na pesa kutimiza malengo yao, wakati wakiwa hawana uwezo wa kutimiza malengo yao wanaacha ndoto zao. Kiukweli unaweza pia kila siku ukafanya jambo moja ambalo linahusiana na ndoto zako, hata kama ni dogo lakini siku yako imepita vyema kwa kuiishi katika ndoto yako.

7. Kujisikia vibaya watu wakikusema vibaya.
Fahamu kuwa watakuhukumu (watahukumu kwa mabaya au kwa mema), kwani wanadamu wengine hupenda kuhukumu watu na kuwazungumzia watu, lakini ukipoteza raha yako kuwaza watakuhukumu vipi utakuwa mtumwa. Sio vibaya kusikiliza watu wanavyokuhukumu, lakini ni vibaya pale mtu anapokuhukumu vibaya na wewe kumchukia, mpende na jifunze uimara kupitia yeye, kwani changamoto hiyo ipo kwa ajili ya kukuweka imara na kuzidi kuongeza upendo kwa wanaokusema vibaya.
Shukuru kwa kila jambo na jiamini. 

8. Kushikilia mambo hasi.
Ni vigumu kuwaza mambo chanya au hasi kwa pamoja, bali unaweza kuwaza au kushikilia moja. Kumbuka mawazo na fikra zako huumba. Pale unapoona unawaza mambo katika upande chanya basi badili mtazamo wako na jaribu kuwaza katika upande wa hasi.

Wengi wanawaza kuwa "ni vigumu kufanya hivi", "Ukifanya hivi utashindwa", "Wewe huwezi", "Unajidanganya" n.k. Mawazo haya hayajengi bali huzidi kukupa hofu. Unapowaza mambo chanya hupelekea mambo chanya kutokea na unapowaza mambo hasi hupelekea hasi kutokea. Kila njia moja ina umuhimu na kila njia inakupeleka katika upande tofauti.

Badala kuwaza mabaya na kushikilia imani duni weka msimamo wako katika njia sahihi. Usikubali kuwaza mabaya wakati wote. Usikubali hofu, wasiwasi, hukumu, maneno, mawazo mabaya yakutawale. 

Unapoweka akili katika mawazo hasi unaipa nafasi ya kukuonyesha njia.

9. Kujilinganisha na wengine.
Kujilinganisha hupelekea "wivu" na "tamaa". Usikubali kujilinganisha na watu wengine, usikubali kuweka tamaa ya kutamani maisha au hali ya mwingine. Sheherekea mafanikio ya mwenzio lakini sio utamani na kutaka kuwa kama yeye, bali jifunze kupitia kwake na wewe uwe kama wewe. Kila mmoja ana safari yake ya maisha, ndio maana uhai ukajigawanya katika personality mbalimbali.
Hata wewe ukijiangalia kuna anayetamani kuwa kama wewe, kuna ambaye hajafika ulipofika wewe, kuwa wewe kama wewe huku ukifurahia mafanikio ya wenzio na sio ushindani, wivu, tamaa n.k.
10. Kutaka Watu Wakukubali Kwa Ndoto Zako.
Usifanye kitu ili watu wakuone mjanja au watu wakusifie bali weka malengo yako kwa nia ya kujiendeleza wewe na kuendeleza wanaokuzunguka. Ukitaka watu wakukubali ukitimiza ndoto zako utakuwa unaishi kama mfungwa. Jikubali kwanza wewe na hakikisha unaishi katika ndoto yako wewe kama wew
Fahamu unataka nini, weka nia kwa unacholenga, na tumia ulichonacho na kila nafasi uliyonayo kufika unapopanga.

Makala  hii imeandikwa na Apolinary Protas wa JITAMBUE SASA . Unaweza kujifunza zaidi kuhusu maisha na mafanikio, kwa kutembelea blog yake www.jitambuesasa.blogspot.com. Kwa mawasiliano zaidi wasiliana naye kwa email jitambuesasa@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.