google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 15, 2015

Kama Na Wewe Utazidi Kung’ang’ania Fikra Hizi, Umaskini Ni Halali Yako.

No comments :
Katika hali ya kawaida, fikra ulizonazo ndizo zinazoamua maisha yako yaweje. Kama unafikiria chanya ni wazi maisha yako yatakuwa ya mafanikio, lakini kama pia utakuwa na fikra hasi nalo hilo halina ubishi ni lazima utaishia kwenye umaskini tena wa kutupwa. Je, wewe binafsi huwa una mawazo gani? Yakukufanikisha au kukwamisha?
Wengi  wanakwamishwa sana na mawazo yao badala ya kuwasaidia. Utakuta ni watu wa kulalamikia sana watu wengine lakini ukija kuchunguza kinachowatesa ni mawazo yao na si kingine. Mara nyingi huwa nashangaa sana hasa pale ninapokutana na watu wengi wakiwa na fikra  kama za kutaka kusaidiwa sana katika maisha yao. Bila shaka umeshawi kuliona hili, tena nina uhakika sana tu.
Hizi ni moja kati ya fikra au mawazo mabovu yanayowarudisha watu wengi nyuma sana kimafanikio. Wengi wanafikra hizi sana za kutaka kusaidiwa badala ya kusaidia. Kila mmoja anakuwa anajitahidi sana kufikiria namna atakavyoweza kusaidiwa na ndugu yake, serikali, mfadhili au tajiri fulani. Ni jambo la ajabu sana kuona watanzania wengi wanafikra kama hizi.
Tangu tukiwa wadogo tumefundishwa kwamba, maana ya ndugu ni kusaidiwa naye, siyo kumsaidia. Tunakuja kujua kuhusu kumsaidia ndugu, pale tunapokuwa watu wazima na kuwa na uwezo ambao unawafanya hao ndugu kutujia kutuomba msaada. Lakini muda wote huwa tunajua kwamba, wajibu wetu ni kusaidiwa.

Kwa hali hiyo, tumejengewa dhana kwamba, serikali inawajibu wa kutusaidia na ndugu na jamaa zetu wapo kwa ajili ya kutusaidia. Hivyo tunasahau kwamba, ni wajibu wetu kusaidia kuliko kusaidiwa.
Kuna msemo maarufu sana duniani ambao uliwahi tolewa na Rais wa zamani wa marekani kwamba, kabla hujauliza nchi yako imekufanyia nini, jiulize wewe umeifanyia kitu gani nchi yako. Msemo huu una mantiki kubwa sana ndani. Lakini pia kabla hujadai ndugu yako akusaidie, jiulize wewe umewahi kumsaidia nani maishani mwako? Kwa kawaida, wasiosaidia wala kujisaidia, ndiyo wanaodai sana kusaidiwa.
Ni jambo la kusikitisha kwamba, kwa kadri siku zinavyozidi kusonga mbele, ndivyo watu wengi wanazidi kuamini kwamba, wajibu wao ni kusaidiwa na kamwe kusaidia hakuwahusu. Kwa hali hiyo, mtu anakwepa kulipa kodi, halafu analaumu barabara haihudumiwi, hakuna dawa hospitalini au hakuna huduma za jamii kwa ujumla.
Kuna watu ambao kazi yao kubwa ni kuwalaumu ndugu zao kwamba, hawataki kuwasaidia, kuilaumu serikali kwamba, haiwajali, bila kujiuliza ni nani aliwaambia kuna kudai haki bila wajibu.
Inabidi kila mmoja atimize wajibu wake, ili kuomba haki kwake liwe ni suala lenye mashiko. Kuomba haki bila kutimiza wajibu ni aina ya ukichaa. Wajibu wa kila mmoja wetu ni kuuliza yeye amesaidia wapi, amemsaidia nani, na amesaidia nini, na siyo amesaidiwa na nani, lini na wapi.
Siyo suala la mzaha kwamba, wengi wanazidi kuwa wataalamu wa kuomba, wataalamu wa kusubiri kusaidiwa wafanyiwe, bila wao kujiuliza mchango wao kwenye kutenda ambayo yatawasaidia wengine hata serikali pia. Kuna haja ya kubadilika kwani tunaelekea kuchelewa. Na ndio maana kama unandelea kung’ang’ania fikra hizi, mafanikio kwako yatakuwa ni ndoto za mchana.
Tuanze kujifunza na kuwafundisha watoto wetu kwamba, wajibu wao ni kusaidia na siyo kusaidiwa. Ni lazima tuwafundishe kwamba, wasione aibu kusaidiwa, lakini wasiishi kwamba, kusaidiwa ndiyo wajibu wao.
Ni lazima tuanze kujifunza kuwajibika badala ya kudai haki kwanza. Kwa kujifunza kuwajibika, tunajikuta tukisaidia badala kuishi kwa kusubiri kusaidiwa.
Nakutakia mafanikio mema na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nami kwa email dirayamafanikio@gmail.com au simu 0713 048035 kwa ushauri na msaada wa haraka.









No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.