google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 5, 2015

Mambo 7 Ya Kujifunza Kutoka Kwa Bilionea Bill Gates.

No comments :
Kwa hakika unapozungumzia wajasiriamali wenye mafanikio makubwa kwenye dunia hii ya sasa huwezi kukosa kumtaja Bill Gates. Kwa mujibu wa jarida la Forbes lililoko nchini marekani, ambalo huzungumzia sana mafanikio ya watu linadai kwamba kwa sasa Bill Gates utajiri wake unafikia dola za kimarekani bilioni 77. Na jarida hilo linamtaja kwa sasa Bill Gates kuwa ndiye TAJIRI wa kwanza duniani.
Swali kubwa ambalo mimi na wewe tunaweza tukaanza kujiuliza ni kwamba, kitu gani ambacho kimemfanya Bill Gates kufikia mafanikio makubwa? Je, ni bahati au akili nyingi alizonazo? Ni rahisi sana kuamini kuwa ana bahati au akili sana, lakini ukweli wa mambo ni kwamba hakuna jibu sahihi kati ya yote hayo mawili iwe bahati au akili nyingi zaidi. Kama yote hayo siyo sasa ni kitu gani kinachosababisha Bill Gates kufanikiwa zaidi?
Haya Ndiyo Mambo 7 Ya Kujifunza Kutoka Kwa Bilionea Na Mfalme Wa Software Duniani Bill Gates:- 
1. Kuwa tayari kujitoa mhanga.
Katika moja ya maandishi yake Bill Gates anadai kuwa, biashara wakati mwingine ni kama mchezo wa bahati nasibu hivyo huwezi kujua kama utashinda au kushindwa. Hivyo anasisitiza ni lazima kujitoa mhanga ili ufanikiwe. Anaendelea kusema kuwa kuna wakati maisha yana vizuizi, kukatishwa tamaa lakini yote hayo utayashinda ikiwa utaamua kujitoa mhanga, mpaka kufanikisha mipango na malengo yako.
Kitu gani cha kujifunza hapa?
Mafanikio sio lelemama yanahitaji kujitoa mhanga na kulipia gharama za kupata mafanikio hayo. Kinyume na hapo itakwa ni ngumu sana kufikia mafanikio.

2. Kuwa king’ang’anizi.
Wakati Bill Gates akianzisha kampuni yake ya Microsoft ambayo kwa sasa imemweka kwenye chati ya utajiri zaidi, kampuni hiyo mwanzoni ili suasua sana. Lakini kitu kikubwa kilimchomfanya Bill Gates afanikiwe mpaka sasa ni kile kitendo cha kung’ang’ania ndoto zake mpaka zikafanikiwa. Alijituma zaidi na kufanya kazi kwa bidii usiku na mchana mpaka akatimiza ndoto zake.
Nini Cha kujifunza hapa?
Hakuna njia ya mkato kufikia mafanikio na inachukua muda kujenga mafanikio makubwa hivyo ni lazima kuwa king’ang’anizi kama nia yako ni kufikia mafanikio makubwa.
3. Jifunze kutokana na makosa.
Bill Gates anadai ipo siri kubwa sana kujifunza pale unapokosea kuliko ukafanikiwa moja kwa moja. Kwa sababu gani anasema hivyo? Kitu anachodai hapa ni kwamba kwenye kukosea akili huwa inafanya kazi zaidi.  Tofauti na kufanikiwa unakuwa unasifiwa tu na usipokuwa makini unashindwa kujifunza mambo ya msingi.
Jambo la kujifunza.
Acha kuchukia makosa yako unayoyafanya, kaa chini ujifunze ili kufikia kilele cha mafanikio.
4. Kuwa na mitazamo chanya.
Kujijengea mitazamo chanya ni kitu cha muhimu katika maisha yako. Hili pia ni jambo ambalo Bill Gates amelisisitizia ili kujenga mafanikio ya kudumu. Ni lazima kujua kuwa utafanikiwa hata kama unaona njia ya mafanikio ni finyu kwako. Unapokosa mtazamo chanya inakuwa ni rahisi kuweza kushindwa hata kwa yale mambo madogo madogo.
Jambo la kujifunza hapa.
Siri kubwa ya mafanikio ipo kwenye kuyachukulia mambo yako chanya na siyo hasi. Kwa kufanya hivyo utafikia mafanikio makubwa sana.
5. Acha kujilinganisha na mtu mwingine.
Pia Bill Gates anasema kila mtu amezaliwa akiwa tofauti na mwingine na hawezi kufanana na mtu yoyote duniani. Kwa hiyo kama wewe ni mtu wa kujilinganisha na wengine sana na unataka kufanana na hao watu basi utakuwa unapotea. Kitu kikubwa unachotakiwa kufanya nikutafuta mafanikio yako mwenyewe na kuachana na tabia ya kujilinganisha.
Jambo la kujifunza hapa.
Jiamini mwenyewe na kubali yale yaliyomo ndani mwako utafikia mafanikio makubwa sana.
6. Kuwa mkarimu muda wote.
Kitu kingine mbacho Bill Gates anatufundisha katika safari yetu ya kuelekea kwenye mafanikio ni kujifunza kuwa wakarimu muda wote. Akiwa na maana maisha kama maisha wakati mwingine hayatabiriki. Leo unaweza ukawa uko juu kesho ukawa chini. Hivyo ni vyema ukaishi kwa kuchukuliana na wengine sawa, kuliko ambavyo ungejifanya wewe ni wewe tu.
Jambo la kujifunza hapa.
Acha kuonyesha kiburi au kujiona juu sana pale unapokuwa na mafanikio. Badala yake chukua jukumu la kuwa mkarimu muda wote.
7. Furahia mafanikio yako na wengine.
Mjasiriamali wa kweli mara nyingi anafurahia mafanikio yake na wengine. Mafanikio anayoyapata yanabaki kuwa siyo yake pekee, bali hata jamii yake inafaidika kutokana kile alichokifanikisha. Hayo sio maneno yangu bali ni maneno ya Bilionea huyu Bill Gates. Kwa hiyo hapa tunaonyeshwa siri nyingine kubwa ya kufikia mafanikio makubwa.
Jambo la kujifunza hapa.
Ni muhimu kuwapa wengine moyo na kuwashirikisha au kufurahia wote pamoja katika mafanikio tunayoyapata. Kwa kufanikisha hili litatusaidia kuachana na ubinafsi.
Hayo ni mambo machache ya kujifunza kutoka kwa billionea huyu. Chukua hatua ya kutendea kazi huku ukielewa wazi ukiamua kufikia mafanikio unayoyataka unaweza. Kitu kikubwa ni uamuzi wako.
Tunakutakia mafanikio mema na kumbuka endelea kuitembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nami kwa email dirayamafanikio@gmail.com au simu 0713 048035 kwa ushauri na msaada wa haraka.



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.