google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 19, 2015

Mambo 6 Ambayo Watu Wasio Na Mafanikio Wanayafanya Kila Wakati.

No comments :
Kitu kikubwa kinachotofautisha watu wenye mafanikio na wale wasio na mafanikio ni fikra, tabia na yale mambo ambayo wanayafanya kila siku. Watu wenye mafanikio yapo mambo ambayo wanayafanya kila wakati na ambayo huwapelekea kufanikiwa kwao. Na watu wasio na mafanikio yapo mambo pia ambayo wanayang’ang’ania kuyafanya na yanapelekea kushindwa kwao.
Kwa hiyo kama katika maisha yako hujafikia viwango fulani vya mafanikio unayoyahitaji, tambua kabisa kuna mambo ambayo umekuwa ukiyang’ang’ania sana na yamekufikisha hapo ulipo. Hivyo, kama unataka kufanikiwa na kutoka hapo ulipo huna haja ya kujilaumu sana, ni kitendo cha kuamua na kuchukua hatua ya kuachana na mambo yanakurudisha nyuma.
Kwa haraka haraka naomba nikutajie mambo ambayo  wasio na mafanikio wanayafanya kila wakati.
1. Kulalamika.
Watu wasio na mafanikio mara nyingi ni watu wa kulalamika sana. Utakuta wanalalamikia hiki mara kile na mwisho hujikuta wakishindwa kuchukua hatua na kubaki kama walivyo. Hili jambo ambalo hulifanya karibu kila siku kwa kulalamikia hata mambo madogo ambayo wanauwezo wa kuyabadili. Na kwa kulalamikia huko sana, hujikuta wakishindwa kufanikiwa.

ACHA KUWAZA HASI KILA WAKATI

2. Kuwaza hasi.
Fikra na mitazamo ya watu wasio na mafanikio mara nyingi zipo hasi sana. Karibia kila kitu wanakiona kwa mtazamo hasi. Hata suala la mafanikio kwao wanakuwa wanaona ni suala la wengine sio lao. Kwa mitazamo hiyo huwafanya wazidi kuona kila kitu hakiwezekani ikiwa pamoja na mafanikio yao. Kwa kuendelea kujenga fikra hasi, hivyo ndivyo ambavyo hujikuta maisha yao wakiyabomoa bila kujijua.
 3. Kupoteza muda.
Kati ya kitu ambacho hakina thamani sana kwa watu wasio na mafanikio ni muda. Matumizi yao ya muda ni mabovu utafikiri wao wana saa 48 kwa siku. Na kutokana na sababu hii ya kupoteza muda hovyo, maisha yao hubaki kuwa ya hovyo. Kwa sababu hakuna wanachokuwa wanakizalisha katika muda mwafaka. Muda mwingi wanakuwa wanapoteza katika mambo ya kipuuzi na yasiyo na maana.
4. Kupuuza.
Siku zote watu wasio na mafanikio maisha yao ni ya kupuuza mambo mengi ambayo kama wangeyafatilia yangewaletea mafanikio makubwa. Ni watu ambao wanapuuza kwa kudharau sana biashara ndogo ingawa hawana. Hiyo haitoshi wanapoteza pesa kwa matumizi yasiyo ya msingi kwa kuona si kitu. Utakuta haya ndiyo maisha yao kwa sehemu kubwa wanaishi kwa kupuuza mambo madogomadogo ambayo baadae yanawarudisha nyuma kimafanikio.
5. Kujenga uadui.
Pia hiki ni kitu ambacho watu wasio na mafanikio wanacho. Mara nyingi ni watu wa kujenga uadui na watu waliofanikiwa. Maisha yao yanakuwa yamejaa roho mbaya ambazo hazitaki kuona wengine wakifanikiwa. Kwa ubinafsi huo wanaoutengeneza mara kwa mara, huwafanya washindwe kujifunza kutoka kwa watu walio na mafanikio. Na matokeo yake hujikuta maisha yao yakizidi kuwa magumu.
6. Kuficha ukweli wa mambo.
Siyo rahisi kwa watu wasio na mafanikio kuweka wazi ukweli wa maisha yao, hata inapotokea pale wanapohitaji msaada wa kweli. Hawa ni watu ambao ni wasiri sana na hujifanya wana mafanikio kumbe hawana. Na Hili ndilo kosa kubwa wanalolifanya ambalo linawatesa na kuwafanya wakose msaada wa kile wanachokitaka katika maisha yao ya kila siku.
Kwa vyovyote vile, maisha uliyonayo sasa, yanatupa picha nzima ya kile unachokifanya mara kwa mara. Ikiwa maisha yako ni ya mafanikio, endelea kung’ang’ania mambo yaliyokupa hayo mafanikio. Lakini, ikiwa maisha yako ni ya kushindwa inabidi ubadili mwelekeo haraka sana na kuacha kushikilia mambo yanayokurudisha nyuma. Kwa kifupi, hayo ndiyo mambo ambayo watu wasio na mafanikio huyafanya sana katika maisha yao.
Tunakutakia mafanikio mema, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika. Kumbuka TUPO PAMOJA.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani ngwangwalu,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nasi kwa:-
Simu; 0713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.