google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 30, 2015

Kama Kila Unachokifanya Kimeshindwa Kukupa Mafanikio, Fanya Kitu Hiki.

No comments :
Inawezekana  umefanya mambo mengi ya kukupa mafanikio, lakini kila ukiangalia umekuwa ukiona kama juhudi zako zimekwenda bure. Karibu kila kitu unachojaribu kukifanya unaona kimeshindikana. Kila ukiangalia hakuna mafanikio  makubwa uliyoyapata.
Ninajua unaweza ukawa unapitia katika hali hii ambayo kwako inakuwa ni ngumu na inakutesa. Kama ni hivyo huna haja ya kukata tamaa sana. Kila kitu kinaweza kubadilika. Ikiwa kama kila unachokifanya kimeshindwa kukupa mafanikio, kitu pekee cha kufanya hapo siyo kukata tamaa kama unavyofikiri, bali ni KUFANYA KAZI KWA BIDII TENA. Hiki ndicho kitu unachotakiwa kukifanya.
Unaweza ukasema ‘ooh mbona mimi najituma sana na nimekuwa nikifanya hivyo siku zote.’ Hilo linaweza kuwa ni sawa kwako, lakini ongeza juhudi zaidi na zaidi kwa namna tofauti mpaka ‘kieleweke’. Hakuna mbadala mwinginwe wa kitu cha kufanya zaidi ya kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii kuliko mwanzo. Kama ulikuwa ukifanya kazi kwa saa 8, unaweza ukaongeza masaa mengine tena ya ziada, hata kama ni mawili.
Hiyo ndiyo siri kubwa inyoweza kukutoa hapo ulipo na kukupa maisha mengine ya kimafanikio. Acha kujihurumia, acha kufikiria kwamba unajitesa. Wewe fanya kazi kwa bidii. Zipo faida na mambo mengi unayoweza kuyapata ikiwa utaongeza juhudi za makusudi tena kwa kila unachofanya.

FANYA KAZI KWA BIDII ZOTE.
Kwanza, itakusaidia sana kukuondolea wasiwasi kwenye maisha yako. Kwa nini hiyo iko hivyo ni kwa sababu. Kila juhudi na uwezo wako wote utakuwa umeweka sehemu moja. Hivyo, hutajilaumu sana kwa matokeo utakayoyapata hata kama siyo ya kuridhisha.
Pili, kufanya kazi kwa bidii kutakusaidia kutatua matatizo mengi. Kama kulikuwa kuna matatizo fulani madogo yalikuwa yanakusumbua itakuwa ni rahisi kwako kuweza kuyapatia majibu yanayotakiwa.
Tatu, kufanya kazi kwa bdii kutakupunguzia msongo wa mawazo. Hiyo yote ni kwa sababu akili yako haitaweza kupata muda wa kufikiria mambo ya ajabu ajabu kwa sabau ya kuchoka. Baada ya kazi kwako itakuwa ni kupumzisha mwili kwa kulala.
Kama nilivyoanza makala haya, kama kila kitu unachokifanya kimeshindikana ongeza juhudi ya kufanya kazi kwa bidii zote kama mtumwa, matokeo mazuri utayapata na mafanikio yatakuwa kwa upande wako.
Nakutakia siku njema na mafanikio makubwa yawe kwako siku zote na kumbuka endelea kujifunza kupitia mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani ngwangwalu,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nasi kwa:-
Simu; 0713 048 035,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.