google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 27, 2015

Usiruhusu Mambo Haya Matatu Yakakuzuia Kufanikiwa.

No comments :
Yapo mambo mengi ambayo mara nyingi yanakuwa yanamzuia binadamu kufikia mfanikio yake. Mambo hayo yapo ambayo tunakuwa tunayajua na tunaweza kuyatawala, lakini mengine tunakuwa hatuyajui, hivyo inakuwa ngumu kuyatawala. Hivyo kwa vyovyote vile kila mtu hukutana na vizuizi fulani katika safari yake  ya kufikia mafanikio.
Kwa kuwepo kwa vizuizi hivi, hapa ndipo utofauti wa maisha huanza kujitokeza. Wapo ambao huwa ni rahisi kushindwa kutokana na vizuizi. Wapo pia ambao huwa ni ving’ang’anizi mpaka kufikia mafanikio yao. Wale ambao hushindwa , kuna wakati hushindwa kwa vizuizi ambavyo naweza kusema wangeweza kuvishinda kama wangekuwa makini kidogo.
Hapa ndipo kipo kiini cha makala haya kilipo. Jaribu kukumbuka kidogo hivi, ni mara ngapi umekuwa umekuwa ukizuiliwa na mambo madogo madogo kufanikiwa? Bila shaka ni mara nyingi. Kuna wakati ulishindwa kutimiza ndoto zako kwa sababu pengine ya visingizio tena visivyo na maana. Utakuta ni sababu ndogo ndogo ambazo umekuwa ukijitengenezea.
Lakini leo ninachotaka kukwambiani hiki, kama unataka kufanikiwa usiruhusu kabisa mambo haya madogo matatu yakakuzuia kufanikiwa:-
1. Kukosolewa.
Acha kushindwa kufikia mafanikio yako kwa sababu ya kugopa kukosolewa. Makosa unayoyafanya yachukulie yawe fundisho kwako la kuweza kukusogeza mbele kufikia mafanikio unayoyahitaji. Acha kusikiliza maneno ya watu wanaozidi kukukwambia kuwa eti huwezi kufanikiwa tena. Hilo sio kweli kwani hakuna mtu anayejua uwezo wako halisi.
Wapo wengi ambao hushindwa kutimiza malengo yao kwa sababu ya kuogopa kukosolewa. Kama kuna jambo unataka kulifanya wewe lifanye. Kama kuna mtu anayekukosoa mwache aendelee kukosoa lakini safari yako izidi kusonga mbele. Hakikisha usizuiliwe na kosa hili dogo na kukufanya ukashindwa kufikia mafanikio yako.

ONDOA HOFU ILI KUFIKIA MAFANIKIO YAKO
2. Wasiwasi/woga.
Wengi ni watu wa wasiwasi ama woga sana na hata wao kuna wakati wanashindwa kuelewa wasiwasi huo hutokea wapi hasa. Utakuta ni watu wa wasiwasi kwa mambo madodogo madogo na ya kawaida kabisa. Kwa mfano akitaka kufanya jambo hili au lile anakuwa na wasiwasi mwingi sana nafsini mwake. Hili ni jambo ambalo kiukweli huwakwamisha wengi kufanikiwa.
Sasa kwa kuwa na wasiwasi huo ambao unakuwa unaujenga kila siku, inasababisha mipango na malengo yako mengi kushindwa kutumia. Wasiwasi ni kitu ambacho kinawafanya watu wengi kushindwa sana kutimiza malengo yao. Hiyo yote ni kwa sababu unapokuwa una woga unasababisha kushindwa kujaribu mambo mengi ya kukufanikisha.
3. Maumivu.
Inawezekana unashindwa kuendeea mbele zaidi ya hapo ulipo kwa sababu ya maumivu uliyonayo moyoni mwako. Maumivu hayo inawezekana uliumizwa baada ya jambo ulilokuwa ukilifanya kushindwa kukuletea mafanikio makubwa au kukupa hasara ya kutosha. Na ikafika mahali ukashindwa kujuani nini cha kufanya.
Haya ni maumivu ambayo kwa namna moja nyingine tunakutana nayo katika maisha. Ni maumivu ambayo hutufanya tushindwe kusonga mbele kila tukikumbuka makosa hayo. Kama upo au ulishapitia hali hii, najua unaelewa ni kitu gani ninacho kiongea hapa. Ili kufanikiwa, usiruhusu maumivu haya yakakufanya ukashindwa kufikia mafanikio yako hata siku moja.
Kumbuka, kwa kuwa na wasiwasi sana juu ya maisha yako, kuogopa kukosolewa na kushikilia sana na maumivu ni mambo madogo ambayo yanaweza kukuzuia  wewe kufikia mafanikio makubwa. Acha kuruhusu hali hii ijitokeze kwako. Kuwa shujaa wa maisha yako.
Dira ya mafanikio inakutakia siku njema na mafanikio makubwa yawe kwako siku zote. Na kumbuka endelea kujifunza kila siku bila kuchoka.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani ngwangwalu,
Kama una maoni, ushauri au changamoto yoyote inayokuzuia kufikia mafanikio yako wasiliana nasi kwa:-
Simu; 0713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.