google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 8, 2021

Hata Kama Hujazoea Kitu Hiki, Chukua Hatua.

No comments :

Kwa mara ya kwanza unapoingia kwenye mahusiano na mtu, unakuwa hujisikii huru sana kuwa naye, lakini baada ya muda una mzoea mtu huyo na kuanza kuona kila kitu kipo sawa kwako.

Kwa mara ya kwanza unapoingia kwenye biashara, unakuwa pia hauko huru sana na biashara hiyo, lakini inafika muda unaizoea biashara hiyo na kuona kila kitu ni cha kawaida. 

Pia kwa mara ya kwanza unapotaka kuanzisha au kuchukua hatua katika jambo lolote, unakuwa haupo huru, lakini ukishaanza tu, unazoea na unaona kawaida kwako.

Hivi ndivyo huwa ilivyo, kwa mara ya kwanza karibu kila mtu huwa hayuko huru kwenye jambo analolianza. Inakuwa hivyo kwa sababu ya hali ya mazoea aliyokuwa ameizoea.

Kutokuwa huru huko kunatakiwa kusikuzuie kitu chochote. Kama ni hatua unatakiwa kuchukua, huko kutokuwa huru kutokana na kitu kipya utakuzoea na kupiga hatua mbele za kimafanikio.

Kuna watu kutokana na kutokujisikia huru sana, wao huwa wanaamua kabisa, kuacha hicho wanachotakiwa kukifanya. Kuamua kutokufanya kisa huna mazoea, ni kosa kubwa sana.

Ni hatari sana kuacha hicho unachotakiwa kukifanya kwa sababu ya kukosa uhuru kidogo, huo uhuru kidogo usikunyime kitu hata mara moja, utazoea na utafanya makubwa ya kutisha.

KITU CHA KUZINGATIA NA KUELEWA, wewe chukua hatua, bila kujali kitu hicho umekizoea au hujakizoea. Kwa kadri unavyochukua hatua, utajikuta unazoea mbele ya safari.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.