google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 21, 2021

Unahitaji Mambo Haya Matatu, Ili Kushinda Changamoto Inayokusumbua.

No comments :

Kati ya kitu ambacho huwezi kukwepa katika safari ya mafanikio yako ni changamoto. Kwa namna yoyote ile ni lazima utaweza kukutana na changamoto, uwe unataka au hautaki, utakutana nazo.

Na ili kushinda changamoto yoyote ile, unahitajika uwe na ufahamu au uelewe mambo matatu ya msingi sana kwako. Kama hautaelewa hayo mambo matatu haiwezekani kushinda hiyo changamoto.

Jambo la kwanza, muda. 

Ili uweze kuishinda changamoto yako, lazima ujipe muda. Haiwezekani changamoto imetokea sasa hivi, na unataka kuishinda muda huu huu, hicho kitakuwa ni kitu kigumu na sio rahisi. Muda unatakiwa ili kushinda changamoto. 

Jambo la pili, juhudi.

Pia mbali na muda inahitajika, juhudi. Ni lazima uweke juhudi sana ili kushinda changamoto yako. Ikiwa utaiendea changamoto yako huku ukiwa unacheka cheka, basi ni ngumu kuishinda changamoto yako. Unatakiwa uweke juhudi haswa ili kushinda.

Jambo la tatu, nguvu.

Unatakiwa uelewe, kuna changamoto ambazo ili kuzitatua, zinahitaji uwekeze nguvu pia. Inawezekana kuna kazi unatakiwa uifanye, sasa kwa kufanya hivyo utaishinda changamoto yako.

Hayo ndio mambo unatakiwa kuyajua na kuyazingatia ili uweze kuishinda changamoto yoyote. Kama usipoyajua mambo hayo huwezi kufanikiwa katika kushinda changamoto yako.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.