google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 11, 2021

Maisha Bora Yanatengenezwa Na Nia Yako.

No comments :

Ikiwa nia yako ni kuumiza wengine, basi hata wewe itafika muda utaishia kuumia kama hao wengine unaotaka kuwaumiza.

Ikiwa nia yako ni kubabaisha, basi hata wewe ni rahisi kuishia kwenye kudanganya danganya ili kupata hicho ukitakacho.

Ikiwa nia yako ni kutoa kwa wahitaji, basi utajikuta na wewe unapokea kama vile utoavyo kwa hao watu wengine.

Ikiwa nia yako ni kufundisha wengine, basi utajikuta unajifunza mambo mengi sana ya kukusaidia pia kimaisha.

Ikiwa nia yako ni kuwakubali wengine, basi utajikuta unaheshimika sana na hao unaowakubali na wengine pia.

Ikiwa nia yako ni kusaidia watu, basi utajikuta unasaidiwa na watu wengi pia kwenye maisha yako bila hata kutegemea.

Ikiwa nia yako ni kufanya maisha ya wengine kuwa ya mafanikio na bora, basi na wewe maisha yako yatakuwa bora vivyo hivyo.

Hauwezi kuikwepa nia yako, hata kama nia hiyo inaenda kwa wengine, lakini nia hiyo uliyonayo itakurudia pia wewe.

Nia yako ni lazima irudi kwako, iwe kwa kufanya maisha yako yaende mbele au yarudi nyuma, lakini nia uliyonayo itakurudia tu.

Unatakiwa ujue nia yako ndio inaamua wakati mwingine ule ubora wa maisha yako, inategemea na nia uliyonayo. 

Kila wakati jitahidi uwe na nia nzuri, hiyo kwa sababu kila nia yoyote ile uliyonayo muda ukifika ni lazima itarudi kwako.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.