google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 18, 2021

Unatakiwa Kujua Kitu Hiki, Ili Kufanikiwa.

No comments :

Jaribu kufikiria jinsi ambavyo ingekuwa inachanganya kwa kiasi kikubwa, kama mchezo wa riadha ungekuwa hauna ule mstari unao onyesha mwisho wake ulipo, yaani mwisho wa kukimbia kwa kila mtu.

Unafikiria ni kivipi wana riadha wangejua wameshinda? Kama ingekuwa hivyo hakuna mstari, basi ungekuwa ni moja ya mchezo usio na maana, kwa sababu mshindi wa haki asingeweza kupatikana.

Kukimbia mbio inakutaka lazima uwe unajua ni wapi unakofika, mstari lazima uone ndio uweke juhudi zako. Kama ingekuwa hakuna mstari basi inawezekana na mashindano hayo yasingekuwepo. 

Ukweli huo uko sawa sawa na kwenye mafanikio. Ikiwa kweli unataka kufika kule unakotaka kufika, lazima ujue mwisho. Mbio za mafanikio zinataka ujue lengo lako linaishia wapi ili ushinde mbio za mafanikio yako.

Unapokuwa unaona kule unakotaka kufika, juhudi zako zinakuwa zinakazana kuutafuta huo mwisho.  Hutakiwi kuzunguka zunguka, unatakiwa kuujua lengo lako vizuri ili kufikia mafanikio yako.

Kwa kifupi, unahitaji kujua kile unachotaka ili kufanikiwa. Unatakiwa kujua mstari wa mwisho wa mafanikio yako ni upi. Kama hujui unachokitaka, utaishia kuishi maisha ya kawaida sana na yasiyo na maana kwako.

 Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.