google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 6, 2021

Ukiwa Na Mambo Haya Mawili, Utajiamini Sana.

No comments :

 


Kujiamini katika jambo lolote unalofanya kunatokana na mambo mawili, hatua unazochukua na changamoto unazokutana nazo. Hayo ndio mambo mawili yanaweza kukupa kujiamini na kutokuogopa.

Unapokuwa unajiamini, unaweza kufanya jambo lolote. Lakini, unatakiwa ujue, kujiamini huko kuna kuja kwa sababu ya jinsi unavyokubalina na changamoto zako na jinsi unavyochukua hatua zako kila siku.

Kama ambavyo misuli inajengwa, halikadhalika pia kujiamini kwako kunajengwa hivyo hivyo, siku hadi siku. Unavyoendelea kuchukua hatua na kushinda changamoto, unashangaa unajiamini sana.

Acha kukimbia au kuogopa changamoto, hizo zinakufundisha nidhamu, ushujaa, ujasiri na kujiamini. Changamoto yoyote ruksa kuja kwako, ikitoka inakupa fundisho kubwa sana kwako na la maana.

KITU CHA KUZINGATIA NA KUFANYA, weka akilini kwamba, kila siku unatakiwa kuchukua hatua juu ya ndoto zako, kwani kujiamini kwako kunatokana na unavyochukua hatua na kushinda changamoto, ni hivyo tu.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.


 

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.