google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 12, 2021

Kama Unaogopa Kuchukua Hatua Kwa sababu Hii, Unajichelewesha.

No comments :

Kama unaogopa kuchukua hatua eti kwa sababu utaaibika, utachekwa au unaogopa kuonekana mjinga, basi wewe ndio utakuwa mjinga kwa kitendo chako cha kutokuchukua hatua za mafanikio yako. 

Kama kweli huchukui hatua kwa sababu ya kuwaangalia watu wanasema au watasema nini, hilo ni kosa kubwa kwako na unajikwamisha kufikia mafanikio yako. Iweje uogope kuchukua hatua kwa sababu ya watu?

Kama upo kwenye jela hiyo, ya kuogopa kuchukua hatua kwa sababu utachekwa au kwa sababu utaonekana mjinga, basi nikwambie maisha yenyewe ndio yatakayo kuaibisha wewe kwa sababu utakuwa huna kitu.

Wale watu wote wanaonekana wajinga, ndio wanaofanikiwa. Wale wote wanaochukua hatua bila kujali watachekwa au wataambiwa nini, hao ndio huwa wanafanikiwa na kufika mbali. Iweje leo hii wewe uone aibu?

Kama bado unaogopa kuchukua hatua kwa sababu hizo za kitoto, nikwambie unajichelewesha na acha woga wa kijinga. Chukua hatua bila kujali watu watasema nini juu yako, chukua hatua bila kujali kama unachekwa.

Narudia tena, maisha yatakuaibisha vibaya sana, kama utakuwa unaogopa kuchekwa eti kwa sababu ya kile unachokifanya. Fanya chochote kile unachotaka bila kuangalia mtu, na UTAFANIKIWA.

 Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.