google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 20, 2021

Kila Unapokutana Na Changamoto, Anza Kufanya Jambo Hili,...

No comments :

Kila unapoingia kwenye kwenye changamoto yoyote ile, kitu cha kwanza akili yako inachowaza, ni mawazo hasi ya kujuta, kujilaumu pengine kulaumu wengine na kujiuliza, kwa nini hii changamoto imetokea.

Hata hivyo, kila inapotokea changamoto, eneo sahihi la kuanzia, badala ya kuwa na hayo mawazo hasi, anza kuanza kwa kushukuru. Hapo ndipo unapoweza kuanzia kupambana na changamoto yako.

Unaweza usielewe sana, lakini unaposhukuru kwa mara ya kwanza kwa sababu ya hiyo changamoto uliyonayo, kunakuwa kunakusaidia akili yako kutafuta njia ya haraka ya kutatua changamoto yako.

Kutokana na imani yako kila unapokutana na changamoto, shukuru kwa kilichotokea, kubali ndio hivyo uko kwenye changamoto, kisha anza kutafuta suluhisho la changamoto hiyo ambayo unayo bila kusita.

Jaribu kitu hiki ninachokwambia, kila unapokutana na changamoto yako anza na kushukuru kabla hujafanya chochote, nakwambia utapata uvumbuzi wa changamoto yako kuliko unavyofikiria.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.