google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 25, 2017

Imani Tatu Unazotakiwa Kuwa Nazo Ili Kukufanikisha.

No comments :
Najua hapo ulipo una mipango au malengo ya aina fulani uliyojiwekea na unahitaji mipango hiyo itimie. Lakini ili kuyafikia hayo malengo yako, mara nyingi huwa hayawezi kutimia mpaka ndani yako ujenge imani tatu muhimu. Hizi ni imani muhimu sana kwa mabadiliko yoyote unayoyataka maishani mwako.
Bila kuwa na imani hizo si malengo peke yake ambayo hayataweza kutimia  hata pia mabadiliko yoyote hayawezi kutokea kama huna imani hizo tatu. Kwa sababu hiyo, hili ndilo lengo la makala haya, ikusaidie kujua aina za imani unazotakiwa kuwa nazo ili kukufanikisha kwa kile unachokihitaji.
Hizi ni imani ambazo unatakiwa kuwa nazo wewe kila siku. Huwezi kufanikiwa sana kama huna au hujajifunza kujenga  imani hizi tatu muhimu kwenye maisha yako.
Bila kupoteza muda fuatana nasi katika makala haya kujifunza pamoja imani tatu unazotakiwa kuwa nazo ili kukufanikisha;-.
1. Lazima uamini maisha yako yanakwenda kubadilika.
Ili uweze kuleta matokeo chanya na kukipata kile unachokitaka ni lazima uamini maisha yako ni lazima yatabadilika. Imani hii ni muhimu sana kwa kwa mabadiliko yoyote unayotaka kuyachukua kwenye maisha yako.
Kama hutakuwa na imani hii itakuwa ngumu sana kuweza kufanikiwa. Hata uwe katika wakati mgumu vipi, lakini ni lazima kwako kutambua maisha yako ni lazima yabadilike.
Kwa kuendelea kuamini hivyo itakupelekea kuchukua hatua ambazo zitakusaidia kufikia ndoto zako. Kama una kitu au hali  unayotaka kuibadili, amini kabisa unakwenda kuibadili hali hiyo au maisha hayo.

2. Lazima uamini wewe ndiye utakayebadii maisha yako.
Hakuna mtu mwingine mwenye uwezo wa kubadili maisha yako zaidi yako. Kama unaisubiri serikali ibadili maisha yako utachelewa, kama unasubiri ajira utachelewa, unatakiwa kuchukua hatua mara moja.
Hakuna mwenye uwezo wa kubadili`maisha yako zaidi ya wewe. Upo ulazima wa wewe kuamini kwamba ndie utakayebadili maisha ako na familia yako na siyo mtu mwngine.
Iwe unakabiliwa na changamioto ya mtaji ni lazima ujue wewe ndiye unatakiwa ubadili hali hiyo. Ikiwa unakabiliwa na changamoto ya hali ngumu ya maisha pia wewe ndiye mwenye uwezo wa kuibadili.
3. Lazima uamini unao uwezo wa kubadili maisha yako.
Pamoja na kwamba umeamini maisha yako yatabadilika na ni wewe ndiye utakayebadili hali hiyo, pia upo ulazima wa kuamini  hali hiyo inawezekana kwako kabisa kubadilika.
Acha kujikatisha tamaa kwa namna yoyote ile. Kila kitu kinaweza kubadilika katika maisha yako na kufikia mafanikio makubwa. Hata hali ya maisha yako nayo pia ina uwezo wa kubadilika.
Kwa kifupi hizo ndizo imani tatu muhimu unazotakiwa kuwa nazo ili kufanikishha jambo lolote lile katika maisha yako.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.