google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 19, 2017

Jiwekee Mkakati Huu,…Ili Ujihakikishie Mafanikio Yako.

No comments :
Katika utoto wake hakuna kitu ambacho alipenda sana kijana huyu kama kuona ndoto yake inatimia. Aliandika vizuri ndoto yake kwenye daftari lake na kisha kila wakati aliipitia ndoto hiyo.
Shauku ya kuona ndoto yake ikitimia alizidi kutokea karibu kila siku. Alitamani kuiona ndoto yake ikitimia mapema sana kwa kadri iwezekanavyo. Kwa kifupi, alikosa raha hasa alipoona kwa nini ndoto yake haitimii?
Hata hivyo pamoja na kuwa na hamasa kubwa ya kuona ndoto yake inatimia ,kijana huyu alikuja kugundua kuna kitu kimoja kinamzuia kufanikiwa. Kitu hicho hakikuwa kingine bali ni shule.
Akiwa na miaka 22 akiwa elimu ya juu aliamua kuachana na shule na kwenda kutimiza ndoto yake aliyokuwa akiifikiri. Lakini hata hivyo kazi haikuwa nyepesi sana kama alivyofikiri.

Jiwekee mpango wa muda mrefu ukusaidie kufikia ndoto zako.
Ingawa kijana huyu alikuwa hana pesa, maskini, hivyo ilimlazima kuanza kuimba kwenye kumbi za starehe, ‘bar’ na ilimlazima wakati mwingine hata kulala vibarazani, lakini alidhamiria kutimiza ndoto yake.
Hali ya kuendelea kuimba huku akiwa katika wakati mgumu aliendelea nayo hivyo hivyo, lakini kuna wakati mambo yalizidi kuwa magumu sana hadi hali iiyopelekea mpenzi wake mpendwa kuachana naye.
Kitendo cha kuweza kuachana na mpenzi wake kilimuuma sana, aliona maisha ndio yamefikia mwisho, hivyo uamuzi pekee aliamua kuuchukua ni kujiua. Maisha yalikuwa hayana maana tena kwake.
Kabla hajachukua uamuzi huo aliamua kwenda hospitali kupima kama akili zake kweli ziko sawa, baada ya majibu na kugundulika kwamba yuko sawa, alikaaa chini na kujiuliza ni nini hasa kinachonifanya nijiue?
Alikuja kugundua huo ungekuwa ni ujinga wa kutupwa. Aliapa na kuamua kwa vyovyote vile itakavyokuwa, hata dunia nzima imtenge ni lazima aitimize ndoto yake. Alikubali kufanya kazi usiku na mchana mpaka kieleweke.
Tokea afanye uamuzi huo, ilimchukua miaka mingine miwili hadi pale angalau alipoanza kuona matunda ya kazi yake. Hapo ndipo alipoanza kukubalika na muziki wake kuanza kufahamika.
Kitu kilichomsaidia ni kule kujitoa kwake na kukubali kuchukua mpango wa muda mrefu kuliko kuota ndoto za kufanikiwa mara moja ambazo zingemuangusha.
Huyu tunaye mzungumzia hapa si mwingine bali ni Bill Joel, moja kati ya wanamziki maarufu duniani. Leo hii angekuchukua maamuzi ya kujiua mara baada ya kuachwa na kushindwa usingeweza kumsikia tena.
Hapa tunajifunza kuna wakati ili kuweza kufanikiwa unahitajika kujiwekea mikakati ya muda mrefu yaani ‘long term plan’. Bila kufanya hivyo ni rahisi sana kushindwa hata pale ambapo hukutakiwi kushindwa.
Kwa lugha nyingine namaanisha ile habari ya kutaka kufanikiwa ndani ya muda mfupi, unatakiwa ujifunze ‘kuizika’ mapema ili ujipe muda mzuri wa kutengeneza mafanikio yako kwa uhakika.
Kile kinachonekana leo kama hakitoi mafanikio kwako makubwa, kitafanikiwa na kukupa mafanikio makubwa endapo utakipa muda na kuendelea kuweka juhudi kila siku na kujifunza.
Maisha yapo kama majira ya mwaka, kuna wakati wa baridi, wakati wa joto au wakati wa upepo. Hivyo unatakiwa kujifunza kukabiliana na nyakati zote hizo ili zikusaidie kuweza kufanikiwa.
Lakini ikiwa ni mtu wa kulia na kuona mambo hayawezekanai kwa sababu umeshindwa au kwa sababu dunia imemekukata utakua ni mtu wa kushindwa sana.
Kila wakati jiandae kuwa kuwa shujaa kwa kile unachookifanya. Achana na habari ya kulialia. Ukiweka msingi na mikakati wa kuwa na malengo ya muda mrefu. Hakuna kitakachokuzuia kufanikiwa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,







No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.