google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 8, 2017

Kinachokufanya Uwe Maskini Ni Hiki…

No comments :
Watu sio maskini eti kwa sababu hawana pesa, watu ni maskini ni kwa sababu ya mawazo yao. Unaweza ukawa unapato zuri sana lakini ukabaki kuwa maskini katika maisha. Kitakachokufanya uwe maskini ni matumizi ya mawazo yako katika kukufanikisha.
Wapo watu wengi sana ambao wana kipato kikubwa lakini wanashindwa kufikia utajiri. Hapo hakuna uchawi wowote ni matokeo ya matumizi ya mawazo. Wataalamu wa mambo ya mafanikio wanatuambia hivi, asilimia 90 ya matatizo yote ya pesa yana sababishwa na matumizi ya mawazo au akili zako.

Hivyo, ni muhimu sana kila wakati kuangalia, je mawazo yako yana uwezo wa kukufikisha kule unakotaka kufika kimafanikio? Ukiona una mashaka hata kidogo, ongeza juhudi ya kujifunza na kutamani kujua kila kitu kinachohusiana na pesa na mafanikio maishani mwako.

Wewe ni tajiri mkubwa sana, ikiwa utajiamini na kukubali kutumia nguvu kubwa ya mawazo uliyo ndani mwako kukufanikisha. Miaka kadhaa mbele naamini utakuja kunitafuta na kuniambia aisee ni kweli ulichosema Imani. Yote hayo yanawezekana kwako, hakuna uchawi zaidi kuchukua hatua na kujituma. 
Tafakari hili kwa kifupi jumapili ya leo na chukua hatua.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,

IMANI NGWANGWALU,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.