google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 23, 2017

Upi Ni Uhusiano Wa Kimazingira Na Mafanikio?

No comments :
Kuna mahusiano makubwa kati ya mafanikio yako na mazingira yanayokuzunguka. Lakini mafanikio hayo huwa hayaji kwa bahati mbaya,  au huwa hayaji kama ajali.  Bali huja kwa kuyatazama mazingira hayo, kama sehemu ya mafanikio yako.  Huenda nikawa nimekuacha kidogo ipo hivi, maana halisi ya neno mazingira ni mjumuisho wa kila kitu ambacho humzunguka mwanadamu. 

Hivyo Moja ya changamoto kubwa ambayo imekuwa ikisababisha maisha ya wengi kuwa katika hali ya ya kawaida ni kutokana na vile ambavyo wameamua kuyachukulia mazingira katika hali ya kawaida pia. Lakini ukweli ni kwamba ili uweze kuwa mtu mwenye mafanikio amini ya kwamba wewe si mtu wa kawaida na mazingira uliyonayo ni ufunguo wa mlango wa mafanikio yako.

Kuwa mtu wa kawaida kumekufanya ushindwe kufikia kusudio lako. Swali linakuja tena kwanini uwe mtu wa kawaida kama kweli unataka mafanikio ya kweli?  Bila shaka majibu yake yasikufanye kuwa ni mtu wa kawaida. Mafanikio makubwa huja kwa mtu ambaye yupo tayari kwa ajili ya mafanikio hayo.

Pamoja na changamoto nyingi ambazo zipo katika dunia hii, changamoto hizo zisikufanye ushindwe kufanikiwa.  Kabla ilivyo ada yangu kukueleza bayana ya kwamba "kukata tamaa ni kosa la jinai" hii ni kwa mujibu wa sheria za mafanikio.


Huenda bado ukawa huamini kama ipo siku utafanikiwa,  ila nataka kukutia moyo kwa kukwambia ya kwamba mafanikio yako yapo upande wako, endapo utaamua leo kuweza kuyatawala mazingira yako vizuri. 

Sheria ya mafanikio na uhusiano wa mazingira inatuambia ya kwamba watu wengi wanashindwa kufanikiwa kwa sababu wametawaliwa na mazingira. Mazingira hayo hayo umewafanya watu wengine wamefanikiwa na wengine bado hawajafanikiwa. Sasa swali linakuja mazingira haya ya nini kwani? 

Tuendelee kidogo kwa kuyazungumza mazingira haya. Mazingira haya endapo utayatazama kwa macho mawili utagundua ya kwamba yametawaliwa na wingi wa changamoto nyingi kuliko fursa. Na endapo utayatazama mazingira hayohayo kwa jicho la tatu utagundua yametawaliwa na fursa nyingi kuliko changamoto.

Unashangaa wala usishangae huo ndio ukweli. Swali la kujiuliza unatumiaje mazingira uliyonayo kama fursa ili uweze kufanikiwa?  Usinipe majibu.  Lakini Ukichunguza kwa umakini utagundua ya kwamba watu wengi tumekuwa tukiyachukulia mazingira ambayo tunaishi katika misingi ya ukawaida na ndo maana tumekuwa siku sote sisi ni wa kawaida. 

Lakini nataka nikuase kwa kusema ya kwamba maisha hayo ambayo unatamani kuwa,  ni lazima uweze kuyatazama mazingira katika sura ya fursa na si changamoto kama ulivyokuwa ukifanya awali.  Hata kama mazingira iliyopo yana changamoto gani, Changamoto hizi unatakiwa kuzikabili kwa kufanya kitu tofauti .  Maana kuna usemi ambao unasema ya kwamba changamoto ni fursa.

Mazingira yanayokuzunguka isiwe kigezo cha wewe kuwa maskini kwani wewe si mtu kawaida,  hivyo yafanye mazingira hayo kama kigezo cha wewe kufanikiwa. Siri ya mafanikio yako ipo katika mazingira yako. 

Nikuache na ujumbe usemao" Mazingira yangu mafanikio yangu "
Ndimi:  Afisa Mipango Benson Chonya,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.