google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 15, 2017

Tiba Na Kinga Asilia Za Maradhi Mbalimbali Ya Kuku.

3 comments :
Linapokuja suala la ufugaji hasa wa kuku kuna wakati zinahitajika dawa nyingi  ambazo inatakiwa zitumike kutibu kuku mpaka waweze kukua vizuri.

Kuna wakati mfugaji kutokana na hali ya kiuchumi hujikuta hana pesa ya kununuliwa dawa za kuweza kutibu kuku wake mpaka wapone.

Sasa kitu cha kujiuliza mfugaji huyu anapokosa pesa anafanyaje wakati kuku wana ugonjwa wa aina fulani?

Jibu ni rahisi tu ni lazima atafute tiba mbadala ili kuwakinga kuku. Kinga zipi mbadala? fuatana nasi leo hii katika makala haya kujua aina ya mimea inaweza kutibu maradhi mbalimbali ya kuku. 

A.  Sehemu za mimea zinaweza kuwa:-

Majani, Magome, Mbegu, Maua au Matunda

B.  Umuhimu wa kutumia tiba zenye asili ya mimea.

Hupatikana kwa urahisi.

Ni rahisi kutumia.

Gharama nafuu.

Zinatibu vizuri.

Hazina madhara.

C.  Baadhi ya mimea inayotibu Maradhi ya Kuku:

1.  Mwarobaini (Majani, Mizizi, Magome).

Hutibu magonjwa yafuatayo:

Typhoid.

Kuzuia Kideri.

Kuhara.

Mafua. 
Vidonda.

Mwarobaini.

 2.  Shubiri Mwitu (Aloe vera).

Chukua majani 3-5 makubwa, katakata na loweka ndani ya maji lita 10 kwa masaa 12 hadi 16. Wape kuku kwa siku 5 - 7.

Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine baada ya masaa 12.

Mchanganyiko huu unaweza kutibu:

Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba/Kitoga/Chinoya/Sotoka)
- inyweshwe kabla kwa kinga.

Homa ya matumbo (Typhoid).

Mafua (Coryza).

Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera). 

Shubiri mwitu.
3. Mtakalang’onyo (Euphorbia).

Chukua Majani makubwa 3-5, ponda, weka katika lita 10 za maji kwa masaa 12-16, chuja na wape kuku. Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine.

Mtakalang’onyo hutibu:

Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba) - inyweshwe kabla kuzuia

Gumboro.

Ndui.

Kuhara damu (Coccidiosis).

Mtakalang'onyo.

 4.  Mbarika (Nyonyo).

Hutibu Uvimbe.

Weka majani ya mbarika ndani ya majani ya mgomba kisha weka ndani ya jivu la moto, kisha kanda sehemu yenye uvimbe kwa kutumia majani hayo ya mbarika.

Nyonyo.

 5.  Mlonge (Mlonje).
Ina vitamini A na C. 

Chukua majani ujazo wa mikono miwili (gao mbili). Kisha yapondeponde na kuyaweka katika lita 10 za maji na iache kwa masaa 12-16, chuja na wape kuku. Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine. 

Mlonge hutibu:

Mafua.

Kideri - inyweshwe kabla kwa kukinga

Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera).

Homa ya matumbo

Ini.
Mlonje.

 6.  Konfrei.

Ina madini na vitamini nyingi.

Hutibu vidonda na majipu.

Konfrei.

 7.  Ndulele (Dungurusi, Makonde, Tura/Ndula).

Majani hutibu Minyoo.

Matunda hutibu Vidonda.

Ndulele.

8.  Papai (Majani).

Chemsha magao mawili ndani ya maji lita 6 hadi ubakie na lita 1. Poza kisha chuja. 

Hutibu: Minyoo

Papai.

 9.  Mwembe.
Majani magao mawili, ponda na chemsha ndani ya lita 6 za maji hadi ibaki lita 1. Wape kwa siku moja.

Mwembe hutibu:

Homa ya matumbo.
Mafua.

Kinga ya Kideri/Mdondo.

Embe.
10. Mpira.

Chemsha majani au mizizi.

Mpira hutibu:

Tumbo

Vidonda na majipu

11.  Minyaa (Cactus).

Hii ni aina yenye majani manene-hadi kufikia nusu nchi na mapana hadi kufikia upana wa viganja viwili vya mikono. 

Minyaa hutibu: (Angalia inaunguza au kubabua).

Vidonda.

Ngozi.

Uzazi.

12. Pilipili Kichaa.
Pondaponda kiasi kisha changanya na maji na wawekee kuku wawe wanakunywa kwa muda wao. Inasemekana inasaidia kutibu Mdonde (lakini mapema kabla maradhi kuingia).


Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.


Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.

3 comments :

Note: Only a member of this blog may post a comment.