google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 23, 2016

Siri 15 Za Kukabiliana Na Changamoto Za Soko Katika Biashara.

No comments :
Watu wengi wanafanya biashara, kulima au kuzalisha mali kwa lengo la kutafuta pesa na maisha mazuri. Lakini je, mteja wetu tunaemzalishia ni nani? Na kile tunachokizalisha kinatupa soko la uhakika? Mara nyingi soko ni tatizo kubwa sana kwa wazalishaji iwe wadogo au wakubwa. Na hili ndilo tatizo kubwa linalosababisha kutokufanikiwa katika biashara au shughuli zetu.

Soko ndio kila kitu katika biashara yeyote ile. Bila soko hakuna biashara na bila biashara hakuna soko. Kama nilivyosema hapo awali tatizo au  changamoto kubwa aliyonayo mkulima, mfugaji,mjasiriamali,mfanyabiashara mdogo na mfanya biashara mkubwa ni soko. Kwa nini tatizo ni soko? Tulia mzee wa nyundo nikupe uhondo leo.

Mara nyingi soko linakuwa ndio tatizo na changamoto  kubwa   kwa watu wote wanaofanya biashara kwa sababu kuu zifuatazo:

1.Kutegemea  wateja wale wale kwa wafanyabiashara wote.

2.Kuzalisha bidhaa zinazofanana kwa wazalishaji wote kama ni mchele ni huo huo wa  mbeya na morogoro unafanana tofauti tunaitengeneza walaji tu ila bidhaa ni ileile.

3. Kutumia mbinu zilezile za kizamani katika kuuza bidhaa hakuna uboreshwaji katika ufungaji au upangaji.

4. Soko ni tatizo kwa sababu watu wengi hawana elimu ya biashara hukurupuka tu kwa kuambiwa na rafiki au kusikia biashara fulani inalipa.

5.Watu wengi hawafanyi utafiti wa soko la bidhaa wanazozalisha huamini nitawapata tu wateja madamu mzigo au mali ninayo na hivyo kujikuta wakipata hasara na kufilisika.

Siri 15 Za Kukabiliana Na Changamoto Za Soko Katika Biashara.
FANYA UTAFITI WA SOKO KABLA HUJAFANYA BIASHARA
6. Watu wengi hufuata mkumbo kwa kufanya biashara kwa kuona jirani au rafiki yake kafanikiwa naye hujidumbukiza bila kutafiti alianzaje? Hizo ndizo sababu za kwa nini soko ni changamoto au tatizo katika biashara.

Ni kwa namna gani tunaweza kutatua hizi changamoto za Soko?
Sasa twende pamoja nikupe siri 15 za kukabiliana na changamoto au tatizo la soko katika bidhaa, huduma na mali unazozalisha.

1. Lazima ufanye utafiti wa kutosha juu ya uhakika wa soko la bidhaa  zako au biashara  nje na ndani kabla ya kuanza kuifanya biashara hiyo.

2. Ni lazima ujue uhitaji wa bidhaa au huduma ya biashara yako ni ya msimu au ya muda wote.

3. Ni lazima ujue wateja wako ni wa aina gani katika kipato chao, kipato cha juu, cha kati au cha chini kabisa ili ikupe uhuru wa kupanga bei.

4. Ni lazima ujue ni muda gani wanahitaji huduma yako.

5. Ni lazima ujue gharama za uzalishaji, usafiri, na faida ama posho yako kabla ya kufanya biashara yako vinginevyo utaambulia hasara.

6. Ni lazima uwe na taarifa sahihi muda wote kuhusu soko kushuka au kupanda.

 7. Ni lazima ujue uwezo wa washindani wako kibiashara ili ujue namna ya kukabiliana nao kiushindani katika soko.

8. Ni lazima uwe na lugha nzuri kwa wateja wako

9. Ni lazima uwe mbunifu kwenye biashara yako ili kuwavutia wateja wapya na wa zamani.

10. Ni lazima utengeneze network ya watu wazuri wa kushirikiana nao katika biashara yako.

11. Ni lazima uzalishe bidhaa na uuze bidhaa zenye ubora na sio bora bidhaa.

12. Ni lazima wakati mwingine uzalishe bidhaa zako kwa ‘order’ usizalishe ilimradi tu unaweza kuzalisha na kwenda kuweka sokoni ukimsubiri mteja ambaye huna maagano naye kama atakuja ama laa.

13.Tengeneza utaratibu wa kumsogezea huduma mteja wako ikiwezekana mpelekee hadi nyumbani kwake ili kumteka akili yake na kumtoza gharama ya usumbufu kijanja bila yeye kujua.

14.Tengeneza utaratibu wa kuwa na mawasiliano na wateja wako na kuwapigia simu kwa lengo la kuchukua ‘order’ za siku inayofuata.

15. Wape motisha wateja wako ili kuwavutia wadumu kwako na kukuletea wateja wengine.

Asante kwa kunifuatilia ubarikiwe sana ni mimi mshirika wako katika mafanikio na siri za mafanikio Shariff H.Kisuda alimaarufu mzee wa nyundo kali.

Karibu na endelea kujifunza maisha na mafanikio kupitia mtandao wako wa DIRA YA MAFANIKIO kila siku.


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.