google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 26, 2017

Nguvu Ya Mtazamo Katika Kushindwa Au Kufanikiwa Kwako.

No comments :
Mtazamo una nguvu ya kubadili hali mbaya inayoonekana na kuwa hali nzuri kabisa. Nguvu yote hiyo ya kubadili hayo inatoka kwenye mtazamo alionao mtu huyo.
Mtazamo unafanya maisha kuonekana ya maana, hata pale ambapo wengi wanaona maisha hayana maana tena na yanachosha.
Mtazamo una nguvu kubwa sana ya kulainisha kile kinachoitwa kigumu na kuonekana kirahisi, hiyo yote ni kazi ya mtazamo.
Unapokuwa upo kati kati ya matatizo, hakuna kitu kingine kinachoweza kukuokoa na kutoka hapo na kuwa na amani zaidi ya kubadilisha mtazamo wako.

Unapobadili mtazamo,  hata kama tatizo lako lilikuwa kubwa sana, tatizo hilo unaona linaanza kulainika na linakuwa linawezekana kutatuliwa.
Wengi wanaoshindwa katika maisha na kuamua kukata tamaa kabisa ni watu ambao mara nyingi wameshindwa kutawala mitazamo yao.
Kiuhalisia unaposhindwa kutawala mtazamo wako na ukajikuta una mtazamo hasi, elewa kabisa maisha yako yatakuwa magumu sana katika kila eneo.
Kwa hiyo unaona kabisa mtazamo una nguvu kubwa sana ya kubadili maisha yako, inategemea tu wewe unautumiaje huo mtazamo wako ulionao.
Ndio kila wakati unashauriwa kukaa na watu chanya, watu ambao wataweza kukusaidia kukujengea mtazamo mzuri wa kufanikiwa.
Kwa hiyo kuanzia sasa hutakiwi kushangaa, unapoona wengine wanafanikiwa na wengine wanashindwa hilo ni swala la mtazamo.
Kwa mfano, utakuta ni watu wanaokaa katika mji mmoja au nchi moja lakini wengine wamefanikiwa na wengine wameshindwa, hapo hakuna kingine zaidi ya mtazamo.
Anguko kubwa la watu linaanza na mitazamo yao. Kwa jinsi unavyokuwa na mtazamo mbovu ndivyo maisha yako yanazidi kuwa mabovu pia.
Lakini mtazamo mzuri una siri kubwa ya kugeuza chochote kuwa mafanikio. Mtazamo mzuri unaweza kugeuza hata maji kuwa almasi.
Mtu mwenye mtazamo mbovu mara nyingi hata apewe fursa nzuri vipi sio rahisi kufanikiwa, kinachomwangusha ni mtazamo wake tu.
Hiyo yote inaonyesha kushindwa kwa wengi kunasabbishwa na mtazamo wake sana, na hapo ndipo ulazima kwa kubadilisha mtazamo unahitajika kwa nguvu zote.
Leo kama unataka kufanikiwa, hebu anza kubadili mtazamo wako ili ukusaidie kwani una uwezo wa kubadili chochote na kuwa kizuri.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.