google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 30, 2017

Njia Ya Mafanikio Yako Ipo Hapa...

No comments :
Mojawapo ya kosa kubwa linalofanywa na watu wengi katika safari ya mafanikio, ni kule kukata tamaa hasa wanapokutana na changamoto.
Kwa kukata tamaa huko kwa sababu tu ya kukutana na changamoto, naweza nikasema ni moja ya kosa ambalo linaweza kukufanya usifanikiwe.
Washindi katika maisha wanajua kwamba, changamoto au kushindwa kwa namna moja au nyingine sio ‘tiketi’ pekee ya kuanza kukata tamaa mapema.
Inapotokea kitu hakijaleta majibu unayoyataka, sio swala la kukimbilia kukata tamaa bali ni kubadilisha njia hadi uweze kufanikiwa.

Inawezekana kabisa njia unazotumia ni butu na hazifai, sasa hapo sio rahisi sana kuweza kufanikiwa, bali kufanikiwa kunakuja kutokana wewe kutumia njia mbadala.
Kama njia ya kwanza imekataa, jaribu ya pili na kama ya pili imekataa, jaribu ya tatu na nyingine na nyingine tena mpaka kuweza kufanikiwa.
Ipo njia ya kukufikiasha kwenye mafanikio yako, njia hiyo ipo. Ili uifikie njia hiyo, acha kukata tamaa mapema. Sumu kubwa sana ya kufanikiwa kwako ipo kwenye kukata tamaa.
Jifunze sana kutokana na matokeo yanayokatisha tamaa na kisha baada ya hapo tafuta njia mpya utakayoitumia kufanikiwa tena.
Kuendelea kufanya tena na tena hata kama unashindwa ni njia muhimu ya kukusaidia kufanikiwa. Kwani amini njia ya mafanikio yako ipo, huhitaji kukata tamaa.
Kama nilivyokudokezea watu waliofanikiwa wanatumia njia nying sana, ambazo njia hizo huwasidia kuweza kufikia mafanikio yao.
Hata wewe unaweza kutumia njia hizo pia. Lakini usiwe mtu wa kukimbilia tu kuacha kila kitu hasa unapokutana na changamoto.
Maisha ya watu wengi yapo hatarini na ni magumu kwa sabbu ni watu wa kuacha tu hasa wanapokutana na changamoto.
Watu hawa hawajafundishwa au hawajui kutumia njia mbadala, ila wao wanachojua ikitokea changamoto dawa ni moja tu ni kuacha.
Ukiwa hata wewe ni mtu wa kuishi maisha ya namna hii, itakuwia vigumu sana kuweza kufikia mafanikio yako makubwa.
Siri ya wewe kufanikiwa unatakiwa kujifunza kufanya jambo kwa namna nyingi sana, ambazo zitakupa mafanikio na sio kukata tamaa kila unapokuatana na changamoto.
Unachotakiwa kuelewa hapa kupitia makala hii ya leo ni kwamba, njia ya mafanikio yako ipo, acha kukimbia mapema kwa sababu ya changamoto. Changamoto zipo na ni za muda.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,                                        
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.