google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 27, 2017

Ukiwa Makini Na Matokeo Haya…Utafanikiwa.

No comments :
Nafikiri na naamini pia, umeshawahi kufanya kitu ambacho haupo nacho makini nacho sana au hutegemei kupata matokeo makubwa kwenye kitu hicho.
Unajua nini kilichotokea wakati unafanya kitu ambacho hukuwa na matarajio nacho sana? ni wazi tu hukufanikinikisha jambo hilo, hicho ndicho kilichokutokea.
Na unajua ni kwa nini hukufanikisha? najua ulikuja na sababu na visingizio vingi sana kwamba umeshindwa kufanya jambo hilo kwa sababu ulizoziweka wewe.
Hata hivyo pia hukufanikisha jambo hilo kwa sababu nguvu ulizokuwa ukiweka hazikuwa nguvu kubwa sana, ulikuwa ukifanya tu kama unacheza na hutilii mkazo.

Kwa hiyo hata unapopata matokeo hayo, hayakukushangaaza sana kwa sababu ni kitu ambacho ulikitegemea kwa kiasi fulani.
Njia na siri ya pekee ambayo inaweza ikakusaidia wewe kutimiza lile lengo unalolitaka au mafanikio uyatakayo ni kuwa makini na matokeo kwanza unayoyahitaji.
Ni rahisi kushindwa kwa chochote kama haupo makini na matokeo unayotaka, kwa sababu kila kitu utafanya kizembe tu, kwa sababu matokeo kwako sio muhimu kivile.
Unapokuwa makini na matokeo unayoyataka,ni wazi utaweka kila aina ya nguvu mpaka kuhakikisha unakipata hicho unachokihitaji bila kuzuiliwa.
Ikiwa hujali sana kile unachokifanya, basi jiulize kwa nini unafanya kitu hicho? Maana hutaweza kuvuna matokeo unayoyahitaji hata kidogo.
Hiyo maanake nini? Unatakiwa uwe na sababu ya kile unachokifanya ili sababu hiyo ikupe nguvu ya kutaka matokeo unayoyahitaji.
Kuanzia leo jifunze kujali sana kile unachokifanya, kifanye kwa ukamilifu na kwa kujali huko utajikuta ukipata matokeo unayoyahitaji.
Hata juhudi unazokuwa unaziweka kwa sababu unajali, zitakuwa ni juhudi zinazokusaidia kwa sababu zinakupa matokeo unayoyahitaji kwenye maisha yako.
Utashindwa na utaendelea kushindwa ikiwa hujali na hauko makini na matokeo ambayo unayahitaji kwenye maisha yako.
Umakini unahitajika sana unatata matokeo yale unayoyahitaji ili uweze kufanikisha chochote kile unachokifanya, tofauti na hapo utakuwa ni mtu wa kushindwa sana.
Nini unachokitaka? Nini unachotaka kukifanikisha kwenye maisha yako? kwa chochote unachokitaka kumbuka, kuwa makini na matokeo, utavuna jinsi unavyopanda.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.