google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 24, 2017

Utajiri Au Umaskini Wako, Unatokana Sana Na Maamuzi Haya.

No comments :
Maisha unayoishi sasa, kwa sehemu kubwa, yanatokana na maamuzi uliyoyafanya kipindi cha nyuma na maisha utakayoishi kesho pia yanategemea sana maamuzi unayoyafanya leo kwenye maisha yako.
Unauwezo wa kuboresha maisha yako kwa kufanya uchaguzi sahihi wa hatua unazozichukua kila siku. Moja ya kitu unachotakiwa uanze nacho ili uweze kuchukua hatua sahihi ni kujifunza juu ya kutawala pesa zako.
Hivi pengine nikuulize, umeshawahi kujiuliza katika maisha yako pesa ngapi zimepita mikononi mwako? Ukiangalia, ni pesa nyingi sana, lakini cha ajabu kwa wengi zimewaacha jinsi walivyo wakiwa hawana kitu.
Sasa basi, ili kuendelea kukosa pesa kusitokee kwako, unahitajika sana kujifunza juu ya kuwa na maamuzi sahihi ya kutawala pesa zako. Ukiipata elimu hii na ukaielewa vizuri, utakuwa umefanya maamuzi sahihi ya kukupeleka kwenye utajiri wako moja kwa moja.
Kwa mujibu wa uchunguzi mdogo uliofanyika unaonyesha hivi, asilimia kubwa ya watu  waliomaskini wanaweka akiba chini ya asilimi 2 na wengine hawaweki kabisa. Hiyo ikiwa na maana kipato chote kinachobakia kinaingizwa kwenye matumizi.
Mpaka hapo kwenye maamuzi hayo, ni moja ya maamuzi mabaya yanayowapeleka wengi kwenye umaskini.  Akiba au kujilipa mwenyewe kiasi kidogo cha kila pesa unayopata ni kitu cha msingi sana kama unataka kesho yako iwe ya mafanikio.
Ni kweli swala la matumizi ya pesa zako liko mikononi mwako, lakini ili uwe tajiri ni lazima ujue namna ya kutawala pesa zako. Sio kwa sababu una pesa unanunua vitu hovyo na kujikuta hakuna hata kiasi kidogo cha pesa ulichobaki nacho.
Angalia usije ukajikuta ukajuta kesho kutokana na maamuzi mabovu unayoyafanya leo juu ya pesa zako.  Fanya maamuzi leo bora yatakayokufanya kesho ukajiona shujaa mkubwa kwa kujiona ulifanya kitu cha maana kwa sababu ya pesa zako.
Ikiwa unataka kuendelea kimaisha na hata kuwa tajiri elewa vizuri juu ya kutawala pesa, yote haya unatakiwa ujifunze ukiwa bado kijana, kama hautafanya maamuzi hayo sahihi, ni wazi hautafanikiwa.
Utajiri au umaskini wako, siku zote upo mikononi mwako kutokana na maamuzi unayoyafanya juu ya pesa. Leo jiwekee kiapo kwamba, kwa pesa yoyote unayoipata ni lazima uweke kidogo kwa ajili yako.
Kwa kuanzia, anza hata na asilimia kumi ya kile unachokipata, umeshindwa kabisa, anza na kiasi chochote. Pesa hiyo kumbuka ni yako, unakuwa haujapoteza popote, hivyo usiwe na wasiwasi, chukua maamuzi sahihi leo yatakaokupa utajiri.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Email; dirayamafanikio@gmail.com.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.