google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 26, 2017

Kama Unashindwa Kufanya Mabadiliko Kwenye Maisha Yako, Basi Tatizo Ni Hili…

No comments :
Kuna wakati unaweza ukajikuta unataka kufanya mabadiliko kwenye maisha yako, lakini unashindwa. Je, umeshawahi kujiuliza kushindwa huko kunatokana hasa na nini au kitu gani. Najua hili linaweza likawa limekotekea.
Ikiwa kila wakati unajaribu kufanya mabadiliko ya kitu fulani na unashindwa kuleta mabadiliko hayo, basi tambua maumivu ya kushindwa hayajawa makubwa sana ndani yako hadi uweze kuleta mabadiliko hayo.
Kwa mfano, unataka kuwa na mtaji na unashindwa kila mara, basi elewa kabisa maumivu ya kushindwa kupata mtaji hayajawa makubwa vya kutosha. Tuchukulie leo hii, ukaambiwa usipokuwa na mtaji hadi mwaka huu unaisha, utapigwa risasi.
Jiulize utakubali kufa kwa sababu ya kukosa mtaji huo unaoutaka? Bila shaka haitawezekana, utafanya kila linalowezekana kufanikisha hilo. Hivyo, wakati mwingine mabadiliko yanakuja kwenye maisha yako kwa sababu ya kule kuumia sana.
Wakati ulipokuwa shule ulisoma sana na kuhakikisha unafaulu ili kukwepa maumivu ya kufeli. Pia kuna wakati umeweka juhudi nyingi sana ili kukwepa maumivu ya aina fulani na kutafuta mahala sahihi kwako.    
Tunaambiwa kitu chenye nguvu ya kubadili tabia yako na mafanikio ni maumivu. Waulize wote ambao wamefanikiwa na ambao wanafikiri chanya kuhusu mafanikio, watakwambia maumivu yamewasaidia sana kubadilika na kuweza kufika hapo walipo mpaka leo.
Hivyo basi, kila wakati tambua hasira ya kushindwa kupata kile unachokita, maumivu ya kushindwa kupata kile unachotaka kukibadili, yatumie maumivu hayo ili yaweze kukusaidia kuweza kufanikiwa.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.