google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 3, 2017

Kwanini Watu Wengine Wanapenda Kukuona Ukiwa Unashindwa?

No comments :
Ni jambo lilowazi kila mtu katika maisha ana harakati za kutafuta mafanikio yake. Pilika pilika za kila siku, zote hizo huonyesha jinsi binadamu anavyosaka mafanikio wakati mwingine hata usiku na mchana.
Pia katika haraka za kutafuta mafanikio, kipo kipindi mbacho kuna wakati tunaweza kusaidiana kwa hili au lile, ili kuweza kutimiza ndoto zetu. Na kuna wakati hata tunapongezana kwa hatua tulizofikia.
Lakini pamoja na kuona wengi wakipongezana kwa hatua walizofikia kimafanikio, bado wapo watu ambao hawataki kabisa kuona wengine wakifanikiwa. Kila wakati elewa kabisa watu hawa wapo, ingawa huwezi kuwajua kirahisi.
Swali la kujiuliza ni kwa nini watu wengine hawapendi kukuona wewe ukiwa umefanikiwa? Je, watu hawa wana roho mbaya? Au shida iliyo ndani mwao ni nini hadi kutotaka wewe usifanikiwe wakati hara wakati mwingine mafanikio yako hayawahusu.

Acha wivu na mafanikio ya wengine.
Jibu ni rahisi tu, watu hawa hawataki ufanikiwe kwasababu , watu huwa wanapoona umefanikiwa kwa kiwango chochote kile, wao wanajisikia vibaya kwa sababu katika maisha yao hakuna walichofanikiwa kikubwa au hawajapiga hatua kabisa pale walipo.
Sasa wanapogundua kwamba unayaendea mafanikio, wakati wao hata hayo mafanikio hawana, wanakuwa wanajisikia vibaya na kutamani tu wewe ushindwe kwa hicho unachokifanya ili muwe sawa.
Jambo hili hutokea sana kwa watu wanaofanya kazi au biashara ya aina moja, watu kila wanapoona mwenzake amefanikiwa kwenye biashara ile ile, hataki kuona akifanikiwa kwa sababu ataona kama atanapitwa vile.
Watu ambao wanachukia mafanikio yako ni wale watu ambao wanaona hawawezi kufanikiwa kama wewe hata iweje. Ujasiri wa kufika sehemu na kuona kama watafanikiwa hawana, ndio maana wanaamua kuchukia kile unachofanikiwa nacho.
Jaribu kujiangalia hata wewe mwenyewe, je kuna wakati inafika unachukia mafanikio  ya watu wengine? Kama ndiyo, unajitengenezea shimo kubwa na kuendelea kushindwa kwenye maisha yako.
Kama unatabia ya kuchukia mafanikio ya watu wengine, achana na hiyo tabia, badala yake anza kujenga tabia itakayokusaidia wewe kuweza kujifunza mafanikio ya hao watu wengine na wewe ukawa kama wao.
Mpaka hapo utakuwa umeelewa vyema kwa nini watu wengine wanachukia kila wakiowaona watu wengine wakifanikiwa.
Endelea kuweka juhudi katika kufikia mafanikio yako makubwa.
 Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.