google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 22, 2017

Watu Wenye Sifa Hii…Ndiyo Wanaofanikiwa.

No comments :
Linapokuja swala la mafanikio zipo sifa na mambo mengi ambayo yanakuwa yanatajwa katika kumfikisha mtu ili aweze kufanikiwa. Mambo au sifa  hizo huwa ni za msingi sana kwa kila mtu ili kufikia mafanikio.
Hata hivyo pamoja na sifa hizo,  ipo sifa moja muhimu sana ambayo kwa mtafuta mafanikio kama unayo ni lazima utafanikiwa. Sifa hii  muhimu ya kimafanikio ambayo nataka kuiongelea hapa ni uvumilivu wako katika kuelekea mafanikio.
Unaweza ukawa unajituma kweli, una nidhamu binafsi na unafanya juhudi za kuwekeza kila wakati, lakini ukikosa uvumilivu hasa pale unapokutana na changamoto au pale unaposubiri mafanikio yako makubwa huwezi kufanikiwa.
Uvumilivu ni kitu cha muhimu sana kama umeamua kuishi maisha ya ndoto zako. Inabidi uvumilie  hali ngumu unazokutana nazo, inabidi uvumilie kuishi wakati mwingine chini ya kipato ili kutimiza malengo ya ndoto zako.
Kuna kitu najua unataka kujiuliza nitavumilia mpaka lini, mbona maisha yangu naona kama magumu, hayaeleweki na hii biashara italeta mafanikio lini? Ndio, najua yote hayo unapitia, hakuna namna zaidi ya wewe kukomaa na kukubali kuvumilia.
Sikiliza, kiuhalisia mara nyingi inachukua miaka 3 hadi 5, ili kuweza kupata mafanikio ya uhakika kwa kile ambacho umekianzisha leo. Huo sio muda mrefu sana kama unavyofikiri. Unachotakiwa kufanya ni kuwa na subira na kuweka juhudi sana kila siku.
Hebu jiulize kuna yale mambo ambayo uliyaanza miaka mitatu iliyopita, yanaonekana kama yalianza jana tu. Kama hiyo iko hivyo hata maisha yako unaweza kuyabadili. Kwa  nini usikubali kuvumulia ili kutengeneza ndoto zako za kimafanikio.
Hata kila unayemwona amefanikiwa, au kila unayemwona yupo ngazi fulani ya kimafanikio kuna mengi ambayo amepitia na kuvumulia hadi akavuna hicho alichokivuna. Kama hutaki kuwa na uvumilivu, utajiweka pembeni kwenye njia ya mafanikio wewe mwenyewe.
Huna haja ya kujiona unachelewa, hebu jipe muda wa kubadili ndoto zako. Uwe na uhakika hilo litafanikiwa na utajenga maisha ya mafanikio unayoyataka wewe. Watu wenye sifa ya kuvumilia magumu mengi na kuweka juhudi hao ndio wanaofanikiwa.
Hakuna hata siku moja mtu ambaye akipata hasara kidogo anaacha biashara eti akafanikiwa, mtu hayupo. Uvumilvu wako ni muhimu sana katika safari ya mafanikio uliyoichagua. Ukiona huna uvumilivu wa kutosha, SAHAU MAFANIKIO.
Tunakutakia kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.