google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 25, 2017

Kitu Pekee Cha Kukiogopa Pale Unapohitaji Mafanikio Ya Kweli.

No comments :

Kuna wakati mwingine inabidi ujutie katika hali ambayo upo hivi sasa, nasema hivyo kwa sababu moja kati ya mambo ambayo inakubidi ujutie katika maisha yako ni kwa sababu umekuwa ni mtu wa kushangaa kuliko kutenda mambo ya msingi.
Tabia hii ya kushangaa kila kitu pasipo wewe kuchukua hatua ndiyo ambayo kiukweli inakufanya uje kujuta hapo baadae, na pia ikumbukwe wakati wewe unazidi kushangaa wapo wengine ambao wanazidi kusonga mbele katika utendaji.
Tabia hii ya kushanga ni mbaya sana katika safari ya mafanikio, kwa mfano, Utakuta wao ni watu wa kushangaa na kuhamasika sana na miradi wanayofanya watu wengine, ukija upande wao hakuna hata kitu kimoja wanachofanya.
Vilevile utakuta watu hawa kazi yao ni  kuingia kundi moja, wanashangaa kinachoendelea humo na kutoka na kuingia tena kundi lingine wanashangaa wee na kutoka tena, pia bila kuchukua hatua, endapo utachukua jukumu la kuwauliza watu hawa watakwambia wanashangaa mataa.
Tabia hii kama unayo ni vyema ukaamua kuiacha mara moja kwani dunia ya sasa hivi ni ya mwendo kasi Zaidi ya kasi ya 4G hivyo kila wakati ni lazima uweze kufanya kazi. Kama kuna fursa hata kama ni ndogo kiasi gani, itumie ikusaidie kufanikiwa na acha kubaki tu kuwa mtu wa kushangaa.  Kama ni kujifunza, jifunze kweli.
Uzuri au ubaya wa maisha hakuna ubabaishaji, ukileta ubabaishaji wa aina yoyote ile, utaumbuka tu na ni lazima utajibiwa na maisha kama vile wewe unavyobabaisha. Badilika rafiki na achana na biashara ya kushangaa, kuwa mtendaji na aamua kufanya kazi.
Hivyo amua sasa kuwa ni mtu wa kuchua hatua kuliko kubaki kushangaa, kwani kufanya hivyo ni kujichelewesha mwenyewe kumbuka ya kwamba kuendelea kushangaa ni kupoteza muda na kupoteza muda ni sawa na kuacha pesa zipite machoni mwako.
Mpaka kufikia hapo hatuna la ziada tukutakie siku njema na mafaniko mema, Mwenyezi Mungu akubariki sana kwa kusoma Makala haya.
Imeandikwa na uongozi wa mtandao blog ya dira ya mafanikio,
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.