google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 25, 2018

Kwa Chochote Unachokifanya Ili Ufanikiwe, Anza Hivi Na Maliza Hivi.

No comments :

Iwe wewe ni shabiki wa kuangalia mchezo wa kukimbia alimaarifu riadha au siyo, lakini kwa vyovyote najua umeshawahi kuangalia mchezo huo hata mara moja na kushuhudia wale washindi wanakuwa wanapatikanaje.
Kama utakuwa umesahau kidogo naomba nitakukumbusha hapa, washindi katika riadha, hususani zile riadha za mita mia moja, wanakuwa wanapatikana kutokana na kuanza kwao kwa kasi na kumaliza kwa kasi.
Hayupo mshindi katika riadha wa mita hasa mia moja kama nilivyosema anayeanza kukimbia kidogo kidogo halafu akawa mshindi kwa madai ya kukazana mwishoni au hakuna ambaye anaanza kwa kasi na mwishoni kukimbia kidogo kidogo na akawa mshindi.
Mchezo huu wa riadha mara nyingi kama unataka ili uwe mshindi ni lazima uanze kwa nguvu, uendelee kukimbia kwa nguvu ukiwa kwenye mbio na wakati huoho umalize kwa kukimbia kwa nguvu sana kwani washindi wanapatikana pale mwishoni.

Hiyo yote inatuonyesha mtu anayeshinda mbio, huwa hapunguzi kasi pale mwishoni bali ndio huongeza kasi, bila kujali anakutana na changamoto za aina gani iwe kuchoka au kuna hata wakati alidondoka, lakini ni lazima kuongeza kasi ili kushinda.
Halikadhalika pia kwa upande wa mafanikio, yanategemea na watu wanaonza kitu chochote kwa nguvu na kumaliza kwa nguvu pia. Kufanikiwa kwa kitu chochote kile ndio kunakuja kwa namna hiyo na sio vinginevyo.
Tatizo hapa la watu wengi wanapoanza jambo fulani wanakuwa wanaanza kwa kasi sana, lakini inapofika katikati ile pumzi yao ambayo wanakuwa wameanza nayo kwa hakika inakuwa inakata hali ambayo hupelekea kushindwa kabisa.
Na kinachokuwa kikipelekea wao kuzidi kupunguza kasi na mwisho kuweza kupotea hapa katika ni kutokana na changamoto, kutokijiamini na wasiwasi ambao wanakutana nao hapa kati kati na mwisho wa siku hujikuta wako nje  ya mstari wa mafanikio.
Unatakiwa ujue mafanikio yanategemea sana wale wote wanaoweka juhudi kuanzia mwanzo na kendeleza juhudi hizo mpaka mwisho wa mafanikio yao. Mafanikio ndivyo yanavyotengenezwa na watu wa namna hiyo.
Kitu pekee ambacho kitakufanya uanze jambo lolote kwa nguvu na umalize kwa nguvu ile ile pasipo hapa wewe kati kati kuweza kupotea kwa namna yoyote ni kujitoa kwako na kujenga mtazamo. Haya mambo yatakusaidia sana.
Unapokuwa umeamua kujitoa na kujenga mtazamo chanya, hapa kati kati hata ukikutana na changamoto nyingi, hutaweza kulalamika zaidi utaongeza mwendo kwa sababu unajua vyema ni wapi unakoenda na unatakiwa umalize vipi ili uwe mshindi.
Nikukumbushe tena washindi katika mafanikio wana anza kwa nguvu, wanaendelea kufanya kwa nguvu na wanamaliza kwa nguvu pia kila wakati. Hii ndio kanuni wanaoyoitumia na wewe unatakiwa uitumie vivyo hivyo pasipo kubabaishwa na kitu.
Kwa chochote ambacho umechagua kukifanya, kianze kwa nguvu, endelea kukifanya kwa nguvu na pia kimalizie kwa nguvu. Usije ukafanya kosa la kuanza kwa nguvu na kumalizia kwa udhaifu, hutashinda ila utashindwa ukifanya hivyo.
Chochote unachokifanya kitakupa ushindi ukiwa utakianza kwa nguvu na kukimalizia kwa nguvu pia. Hakuna hali au mazingira ambayo yatakuzuia kufanikiwa kama moto ule ule ulionanza nao na ndio huo utakaomaliza nao.
Amua sasa kuwasha moto wa mafanikio yako kuanzia mwanzo hadi mwisho, pasiwepo kitu chochote hapa kati ambacho kitaweza kujitokeza na kuzima moto huo. Wewe ni mshindi, anza kwa nguvu, endelea kufanya kwa nguvu na maliza kwa nguvu.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
MUHIMU ZAIDI; kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,







No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.