google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 19, 2018

Mambo Ambayo Huwezi Kuyakwepa Unapotafuta Mafanikio Yako.

No comments :

Katika safari ya mafanikio, yapo mambo ambayo huwezi kuyakwepa hata ufanyaje, mambo hayo ni lazima ukutane nayo. Kuna wakati mambo hayo yanakuwa yanakatisha tamaa sana usipokuwa makini yanaweza kukuangusha. Leo nataka tuyazungumzie mambo haya ambayo huwezi kuyakwepa kwenye safari ya mafanikio yako;-
1. Kupoteza baadhi ya marafiki.
Unapatafuta mafanikio yako kuna wakati unatapoteza marafiki zako ambao unaona hamuendani. Sio marafiki wote mtaokaoweza kwenda nao kwenye safari ya mafanikio. Kuna marafiki utawapoteza kwa sababu hawakusaidii kuweza kufikia kule unakotaka. Inapotekea hivyo usishangae huo ndio ukweli, hakuna namna  zaidi ya kuachana nao.
2. Kufikiri kama unachanganyikiwa.
Kuna wakati vitu vinakua vingi sna kichwani mpaka unaoana kicwa kinawaka moto au unahisi kama vile unachanganyikiwa. Hizi ni hali zinatokea sana kwa mtu yeyote ambaye ni mtafuta mafanikio.  Ukiona kila wakati umetulia na kichwa hakikusumbui, utambue bado hujafikia hatua hiyo ya kutafuta mafanikio yako kwa kasi.

3. Kupatwa na maumivu.
Huwezi kukwepa kukutana na maumivvu unapotafuta mafanikio yako. Kuna wakati utakutana na maumivu ya kukataliwa, kuna wakati utakutana na maumivu ya kupata hasara. Huu ni mojawapo ya mlolongo mchache wa maumivu ambayo unaweza kukutana nayo kwenye safari  ya kutafuta mafanikio yako.
4. Kupoteza pesa.
Upo wakati utafika utapoteza hata pesa zako ikiwa kama hujapoteza. Hilo ni jambo mojawapo pia ambalo unatakiwa ulijue kwamba lipo kwenye safari ya mafanikio yako.  Unapopoteza pesa zako, tafadhari usikate tamaa, hiyo ni dalili tosha ya mafanikio mengine makubwa yanakuja kwako, kikubwa ongeza juhudi na tafuta pesa zingine.
5. Kukatishwa tamaa.
Kipo kipindi wakati unatafuta mafanikio yako utakatishwa tamaa na rafiki zako, ndugu zako na hata mumeo au mkeo kwamba ndoto hizo haiwezekani kwako kuweza kuzifikia. Yote hayo unapaswa kuyajua kwamba yanaweza yakakutokea na hutakiwi kukata tamaa, unatakiwa ujue hali hiyo ipo na unatakiwa kupambana nayo.
6. Utakuwa unajitilia shaka sana.
Pia ni lazima utafika wakati utakuwa unajitilia shaka kwa kuona kwamba huwezi kitu. Kila unapoangalia ndoto zako na kuona ni kubwa unakuwa unawaza sana kwamba ‘kweli nitaweza hili.’ Lakini hapa naomba nikwambie unaweza, haijalishi umejitilia shaka mara elfu moja lakini unao uwezo wa kuweza kusonga mbele kwenye maisha yako.
7. Utakosolewa sana.
Wakati unatafuta mafanikio kuna muda utafika kila unachotaka kufanya unakosolewa na wengine kwamba kitu hicho hakifai. Usipokuwa makini utakuwa unaacha kila kitu kwa kusikiliza maneno ya watu wa nje. Kikubwa hapa iamini ndoto yako na usisikilize mtu kwamba huwezi hili au lile, wewe jiamini na fanya.
8. Utashambuliwa bila sababu.
Kuna watu watajitokeza watu kukutuhumu wewe ni mtu wa kudhulumu, au wewe pesa zako unatafuta kwa njia ambazo sio halali.  Na watakwambia maneno mengine mengi, lakini ukweli utakuwa unaujua wewe ni kipi ambacho unakifanya, kwa hiyo unatakiwa usimame imara pasipo kuteteleka kwa kusikiliza maneno ya watu.
Haya kwa kifupi ni baadhi ya mambo ambayo ni lazima ukutane nayo katika safari yako ya mafanikio. Mambo haya yanapojitokeza kwako yasikukatishe tamaa hata kidogo bali yakupe chachu ya wewe kuweza kusonga mbele. Watu wenye mafanikio wanakabiliana sana na mambo kama haya na mwisho lakini hushinda.
Fanyia kazi mambo haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Nakukumbusha pia, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,








No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.