google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 5, 2018

Tafuta Kitu Hiki Kwanza, Kabla Hujakimbia Changamoto Zako.

No comments :
Pale inapofika mahali unaona umekwama na huoni njia ya kukupeleka mbele, suluhisho hapo kwako usijaribu kutafuta njia ya kurudi nyuma, tafuta njia nyingine ya mafanikio itakayokuwezesha kufanikiwa.
Inapofika mahali pia unaona umekata tamaa na umekatishwa tamaa karibu na  kila kitu katika dunia hii, usisijaribu kuruhusu kweli kukata tamaa huko, tambua ipo njia nyingine ya kukusaidia tena kufanikiwa kwako.
Ikiwa kuna mtu amekuumiza na unajisikia kulipa kisasi, pia nikwambie hilo sio suluhisho sahihi, unatakiwa kujua jinsi ya kukabiliana na hali hiyo lakini si kulipa kisasi kama ambavyo unataka ufanye, unatakiwa kutafuta njia nyingine nzuri ya kulipa kisasi.

Inapofika wakati na ukaona kabisa uchaguzi pekee ulionao kwa kile unachotaka kukifanya ni uchaguzi hasi, unatakiwa kuachana na uchaguzi huo mara moja na kufuata chaguzi sahihi yaani uchaguzi chanya utakaokupa matokeo mazuri.
Kwa kawaida tunakuwa tuna chaguzi nyingi sana mbaya, chaguzi ambazo inafika wakati zinatuangusha wenyewe. Unapaswa kuelewa unashindwa kwenye kitu kimojawapo, chagua njia nyingine ya kukufanikisha.
Unapaswa kukumbuka, kila unapokuwa katika wakati mgumu, wakati ambao unaona wewe huwezi tena kuendelea mbele, kunakuwa kuna njia nyingine ya kukusaidia kuweza kuendelea mbele, hiyo inaeleweka.
Watu wengi wanajikuta wanashindwa sana kwenye maisha yao kwa sababu pale wanaposhindwa kuona mafanikio badala ya kutafuta hatua za kuwawezesha kwenda mbele, utakuta wao wanatafuta hatua za kuweza kukimbia.
Hutakiwi kukimbia changamoto yoyote au kufanya kitu chochote ambacho kinakufanya urudi nyuma. Kila wakati unatakiwa kutafuta njia ya kukuwezesha kuendelea mbele na si kurudi nyuma au kutoroka changamoto.
Kama kuna watu wanatoroka changamoto zao waache wafanye hivyo lakini isiwe wewe. Amua kabisa wewe kuwa mtu wa kutafuta njia ya mafanikio hata pale ambapo njia hiyo inaonekana kama haipo.
Kwa kutafuta njia hiyo, milango mingine ya fursa utashangaa unaanza kuiona na kupelekea njia ya mafanikio ionekane kwa uwazi. Hakuna kinachoshindikana kila kitu kinawezekana, ikiwa utaamua kuitafuta njia ya mafanikio yako.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,






No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.