google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 15, 2018

Mbinu Za Kujitengenezea Maisha Mengine Nje Ya Ajira.

No comments :

Inawezekana ukawa umeajiriwa na miaka nenda na miaka rudi hujawahi kufanya kitu cha msingi, au inawezekana bado umeajiriwa na unasubiri mafao tu. Ninachotaka kukwambia ni kwamba ni lazima uwe na akili nyingine ya ziada itakayokufanya uweze kutengeneza maisha mengine zaidi ya ajira uliyonayo.
Na hayo maisha mengine ili uweze kuyaishi hayo unaweza kujikita katika kufanya biashara au kujiingiza katika suala zima la kufanya ujasiliamali. Haiwezekani ukaendelea kuishi kwenye ajira tu peke yake miaka nenda rudi, kipo kipindi uwe na uhakika utakwama kama usipoingia kwenye ujasiriamali.
Na ili uweze kufanya hivyo unatakiwa kufanya mambo yafutayo;-

1. Dhibiti matumizi yako ya pesa.
Moja kati ya matatizo ambayo yanayowakumba watu waliojariwa ni kwamba wanashindwa kudhibiti matumizi yao ya fedha, Wengi wao wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu wana imani hata pesa ikisha mwisho wa mwezi wana uhakika wakupa pesa nyingine.
Kwa minajili hiyo ndio maana watu hao wanashindwa kuanzisha miradi ya msingi na hivyo kupelekea watu wao kuwa na matumizi mengi ya pesa. Hivyo ili uweze kuanzisha mradi wako ukiwa umejiliwa hakikisha unadhibiti kiwango chako cha matumizi ya pesa katika kila mshahara unaopata.
2. Usitegemee kipato kimoja.
Jambo la pili ni kwamba ukiwa bado umeajiliwa hakikisha ya kwamba hutegemei kipato kimoja cha kukupatia pesa, bali kuwa na vyanzo vingi vya kuweza kujingizia kipato wewe mwenyewe. Ili kufanya hivyo ni vyema ukajikita katika masuala ya ubunifu na ujasiliamali kwa ujumla.
Kubaki na kipato kimoja ni hali ya hatari sana kwako. Unatakiwa una vipato vingi ambavyo vitakuwezesha wewe kuweza kuishi maisha nje ya ajira. Ikiwa hautafanya hivyo itabaki kwako hadithi ya kutokufanikiwa. Ni muhimu sana kutengeneza vyanzo vingi vya pesa ili kuishi maisha nje ya ajira.
3. Tumia mshahara kuanzisha mradi.
Katika hili ni kwamba ili uweze kujitengezee maisha mengine nje ya ajira, kwa hicho kiwango kidogo au kikubwa cha mshahara unachokipata hakikisha ya kwamba unatenga asilimia fulani kwa jinsi utavyoona wewe ili kuanzisha mradi wako binfsi itakayokufanya ufurahie maisha unayoishi.
Mpaka kufikia hapo hatuna na ziada tukututane tena siku nyingine hapa DIRA YA MAFANIKIO kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Ndimi afisa mipango Benson Chonya,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.