google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 31, 2017

Nguvu Ya Nidhamu Binafsi Katika Kufikia Malengo Yako.

No comments :
Ili kufikia mafanikio yako, kati ya kitu ambacho kinahitajika sana ni uwezo wa kujenga nidhamu binafsi ambayo inaweza kukuongoza hadi kuweza kufikia malengo yako. Wapo watu ambao wanakwama sana kutokana na kukosa nidhamu binafsi ambayo inatakiwa iwaongeze katika kufikia malengo yao.
Hivyo hapa unaona, nidhamu binafsi siku zote inasimama kama daraja la kuunganisha pale ulipo na kule unakotaka kufika kutokana na malengo uliyojiwekea. Hiyo ikiwa na maana kwamba, kama huna nidhamu binafsi huwezi kufikia malengo hayo, maana utakuwa ni kama mtu ambaye anayebomoa daraja lako mwenyewe.
Kila unapojiwekea malengo yako ya aina fulani na kisha ukaamua kuweka nidhamu binafsi ya kuyafanyia kazi malengo hayo kila siku hata kama kwa kidogo sana, uwe na uhakika ni lazima utafanikiwa. Kitachokufanikisha hapo ni nidhamu binafsi uliyonayo, hasa ya kuweka juhudi kila siku ambapo umeamua kuiweka.

Unapojiwekea nidhamu binafsi ya kitu chochote na kudhamiria kwamba hutafanya kitu hiki au kitu kile mpaka malengo yako ya aina fulani yatimie, utakuwa upo kwenye uwezekano mkubwa sana wa kutimiza malengo yako. Ila unapokuwa unakosa nidhamu binafsi ni rahisi sana kuweza kushindwa.
Kuanzia leo amua kuweka nidhamu kwenye kila eneo. Weka nidhamu kwenye eneo la pesa, hakikisha pesa zako hazipotei hovyo. Weka nidhamu binafsi kwenye kazi yako. Weka nidhamu kwenye matumizi ya muda wako, ili uutumie kwa faida. Kila eneo muhimu liwekee nidhamu binafsi na utapata matokeo mazuri.
Hata hivyo ukumbuke unapojiwekea nidhamu binafsi sio adhabu au unajitesa. Huwezi kufanikiwa kama unaishi maisha kama unavyotaka wewe. Ipo misingi ambayo unatakiwa uifate ili kufanikiwa ikiwa na pamoja na swala la kujiwekea nidhamu binafsi. Kufanikiwa kwako kutakuwa lazima kama utafata nidhamu hii.
Ndio maana usishangae kuona watu wengi wanashindwa katika maisha, hii sio kwa sababu hawana uwezo au vipaji, yote hiyo ni kwa sababu ya kukosa nidhamu ndogo ndogo ambazo zingeweza kuwaongza katika kufikia mafanikio yao. Ukijiwekea nidhamu binafsi, tambua utafanikiwa tu, hakuna ubishi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.